1属灵的恩赐
1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2你们知道,你们还是教外人的时候,总是受迷惑被引诱,去拜那不能说话的偶像。
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3所以我要你们知道,被 神的灵感动而说话的人,没有一个会说“耶稣是可咒诅的”;除非是被圣灵感动,也没有人能说“耶稣是主”。
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4恩赐有许多种,却是同一位圣灵所赐的;
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5服事的职分有许多种,但是同一位主;
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6工作的方式也有许多种,但仍是一位 神,是他在众人里面作成一切。
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7圣灵显现在各人的身上,为的是要使人得着益处。
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8有人借着圣灵领受了智慧的言语,又有人靠着同一位圣灵领受了知识的言语,
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9又有人因着同一位圣灵领受了信心,还有人因着这位圣灵领受了医病的恩赐,
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10另有人可以行神迹,另有人可以讲道,另有人可以辨别诸灵,也有人能说各种的方言,也有人能翻译方言。
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11这一切都是这同一位圣灵所作的,他按照自己的意思个别地分给各人。
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12正如身体是一个,却有许多肢体,而且肢体虽然很多,身体仍是一个;基督也是这样。
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13我们无论是犹太人,是希腊人,是作奴隶的,是自由的,都在那一位圣灵里受了洗,成为一个身体,都饮了那一位圣灵。
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14原来身体有许多肢体,并不是只有一个肢体。
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15假如脚说:“我不是手,所以我不属于身体。”它不能因此就不属于身体。
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16假如耳朵说:“我不是眼睛,所以我不属于身体。”它也不能因此就不属于身体。
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17假如整个身体只是眼睛,怎样听呢?假如整个身体只是耳朵,怎样闻味呢?
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18但现在 神按照自己的意思,把肢体一一放在身体上。
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19假如所有的只是一个肢体,怎能算是身体呢?
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20但现在肢体虽然很多,身体却只是一个。
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21眼睛不能对手说:“我不需要你。”头也不能对脚说:“我不需要你们。”
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
22相反地,身体上那些似乎比较软弱的肢体,更是不可缺少的。
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23我们认为身体上不大体面的部分,就更加要把它装饰得体面;不大美观的部分,就更加要使它美观。
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24我们身体上美观的部分,就不需要这样了。但 神却这样把身体组成了:格外地把体面加给比较有缺欠的肢体,
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25好使肢体能够互相照顾,免得身体上有了分裂。
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26如果一个肢体受苦,所有的肢体就一同受苦;如果一个肢体得荣耀,所有的肢体就一同快乐。
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27你们就是基督的身体,并且每一个人都是作肢体的。
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28 神在教会里所设立的,第一是使徒,第二是先知,第三是教师,其次是行神迹的,再其次是有医病恩赐的,帮助人的,治理事的,说各种方言的。
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29难道都是使徒吗?都是先知吗?都是教师吗?都是行神迹的吗?
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30都是有医病恩赐的吗?都是说方言的吗?都是翻译方言的吗?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31你们却要热切地追求那些更大的恩赐。现在我要把更高的道路指示你们。
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.