聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 Corinthians

4

1基督的使徒遭人轻视
1Mtu na atuone sisi kuwa ni watumishi wa Kristo tuliokabidhiwa siri za mungu.
2对于管家的要求,就是要他忠心。
2Kinachotakiwa kwa yeyote yule aliyekabidhiwa kazi ni kuwa mwaminifu.
3我被你们论断,或被人间法庭审判,我都认为是极小的事,连我自己也不论断自己。
3Kwangu mimi si kitu nikihukumiwa na ninyi, au na mahakama ya kibinadamu; wala sijihukumu.
4我虽然问心无愧,却不能因此自以为义,因为判断我的是主。
4Dhamiri yangu hainishtaki kwa jambo lolote, lakini hiyo haionyeshi kwamba sina lawama. Bwana ndiye anayenihukumu.
5所以时候还没有到,你们不要批评,直等到主来;他要照出黑暗中的隐情,显明人心里的动机。那时,各人要从 神那里得着称赞。
5Basi, msihukumu kabla ya wakati wake acheni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayafichua mambo ya giza yaliyofichika, na kuonyesha wazi nia za mioyo ya watu. Ndipo kila mmoja atapata sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
6弟兄们,我为你们的缘故,拿了这些事来比拟自己和亚波罗,让你们在我们身上学到的,不会超过圣经所记的,免得你们中间有人自高自大,看重这个轻视那个。
6Ndugu, hayo yote niliyosema juu ya Apolo na juu yangu, ni kielelezo kwenu: kutokana na mfano wangu mimi na Apolo nataka mwelewe maana ya msemo huu: "Zingatieni yaliyoandikwa." Kati yenu pasiwe na mtu yeyote anayejivunia mtu mmoja na kumdharau mwingine.
7使你与人不同的是谁呢?你有什么不是领受的呢?既然是领受的,为什么要自夸,好像不是领受的呢?
7Nani amekupendelea wewe? Una kitu gani wewe ambacho hukupewa? Na ikiwa umepewa, ya nini kujivunia kana kwamba hukukipewa?
8你们已经满足了,已经丰富了,不需要我们,自己作王了。我恨不得你们真的作了王,让我们也可以跟你们一同作王!
8Haya, mmekwisha shiba! Mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme bila ya sisi! Naam, laiti mngekuwa kweli watawala, ili nasi pia tuweze kutawala pamoja nanyi.
9我想 神是把我们作使徒的列在最后,好像定了死刑的人,因为我们成了一台戏给宇宙观看,就是给天使和世人观看!
9Nafikiri Mungu ametufanya sisi mitume tuwe watu wa mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kuuawa, maana tumekuwa tamasha mbele ya ulimwengu wote, mbele ya malaika na watu.
10我们为基督的缘故,成了愚笨的;你们在基督里,倒成了聪明的。我们软弱,你们倒强壮;你们受人尊敬,我们倒被轻视。
10Sisi ni wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara katika kuungana na Kristo! Sisi ni dhaifu, ninyi ni wenye nguvu. Ninyi mnaheshimika, sisi tunadharauliwa.
11直到现在,我们还是又饥又渴,衣不蔽体,又挨打,又没有栖身的地方,
11Mpaka dakika hii, sisi tuna njaa na kiu, hatuna nguo, twapigwa makofi, hatuna malazi.
12并且劳苦,亲手作工。被人咒骂,我们就祝福;遭受迫害,我们就忍受;
12Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;
13被人毁谤,我们却好好地劝导;直到现在,人还是把我们当作世上的垃圾,万物的渣滓。
13tukisingiziwa, tunajibu kwa adabu. Mpaka sasa tumetendewa kama uchafu wa dunia; na kwa kila mtu sisi ni takataka!
14我写这些话,不是要叫你们羞愧,而是把你们当作我亲爱的儿女一样劝戒你们。
14Siandiki mambo haya kwa ajili ya kuwaaibisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwafundisheni watoto wangu wapenzi.
15纵然你们在基督里有上万的启蒙教师,可是父亲却不多,因为是我在基督耶稣里借着福音生了你们。
15Maana hata kama mnao maelfu ya walezi katika maisha yenu ya Kikristo, baba yenu ni mmoja tu, kwani katika maisha ya Kikristo mimi ndiye niliyewazaeni kwa kuihubiri Habari Njema.
16所以我劝你们要效法我。
16Kwa hiyo, nawasihi: fuateni mfano wangu.
17因此,我打发提摩太到你们那里去。他是我在主里亲爱又忠心的儿子,他要提醒你们我在基督里是怎样行事为人,正如我在各处教会中所教导的一样。
17Ndiyo maana nimemtuma Timetheo kwenu. Yeye ni mtoto wangu mpenzi na mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia ninayofuata katika kuishi maisha ya Kikristo; njia ninayofundisha kila mahali katika makanisa yote.
18有人以为我不会到你们那里去,就自高自大。
18Baadhi yenu wameanza kuwa na majivuno wakidhani kwamba sitakuja tena kwenu.
19然而主若愿意,我很快就要到你们那里去;到时我要知道的,不是那些自高自大的人所讲的,而是他们的能力。
19Lakini, Bwana akipenda, nitakuja kwenu upesi; na hapo ndipo nitakapojionea mwenyewe, sio tu kile wanachoweza kusema hao wenye majivuno, bali pia kila wanachoweza kufanya.
20因为 神的国不在乎言语,而在乎权能。
20Maana Utawala wa Mungu si shauri la maneno matupu, bali ni nguvu.
21你们愿意怎么样呢?要我带着刑杖到你们那里去,还是以温柔的灵,带着爱心去呢?
21Mnapendelea lipi? Nije kwenu na fimbo, ama nije na moyo wa upendo na upole?