1祭过偶像的食物的问题
1Yahusu sasa vyakula vilivyotambikiwa sanamu: Tunajua kwamba sisi sote tuna ujuzi, lakini ujuzi huo huwafanya watu wawe na majivuno; lakini mapendo hujenga.
2如果有人自以为知道些什么,那么,他应该知道的,他还是不知道。
2Anayefikiri kwamba anajua kitu, kwa kweli hajui chochote kama inavyompasa.
3如果有人爱 神,这人是 神所知道的。
3Lakini anayempenda Mungu huyo anajulikana naye.
4关于吃祭过偶像的食物,我们知道世上的偶像算不得什么,也知道 神只有一位,没有别的神。
4Kwa hiyo, kuhusu vyakula vilivyotambikiwa sanamu, twajua kwamba sanamu si kitu duniani; twajua kwamba Mungu ni mmoja tu.
5虽然有被称为神的,无论在天上或在地上(就如有许多的“神”许多的“主”),
5Hata kama viko vitu viitwavyo miungu duniani au mbinguni, na hata kama wako miungu na mabwana wengi,
6然而我们只有一位 神,就是父;万物都是从他而来,我们也为了他而活。我们也只有一位主,就是耶稣基督;万物都是借着他而有的,我们也是借着他而有的。
6hata hivyo, kwetu sisi yuko Mungu mmoja tu: Baba, Muumba wa vyote, ambaye kwa ajili yake sisi tuko. Pia yuko Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, na sisi twaishi kwa njia yake.
7不过,这种知识不是人人都有的。有些人直到现在习惯了拜偶像的事,因此他们吃的时候,就把这些食物看作是真的献过给偶像的;他们的良心既然软弱,就被污秽了。
7Lakini, si kila mtu anao ujuzi huu. Maana wako watu wengine waliokwisha zoea sanamu, watu ambao mpaka hivi sasa wanapokula vyakula huviona bado kama vyakula vilivyotambikiwa sanamu. Na kwa vile dhamiri zao ni dhaifu, hutiwa unajisi.
8其实食物不能使我们亲近 神,我们不吃也无损,吃也无益。
8Lakini chakula hakiwezi kutupeleka karibu zaidi na Mungu. Tukiacha kukila hatupungukiwi kitu, tukikila hatuongezewi kitu.
9然而你们要谨慎,免得你们这自由成了软弱的人的绊脚石。
9Lakini, jihadharini: huu uhuru wenu usiwafanye walio na imani dhaifu waanguke katika dhambi.
10因为如果有人看见你这有知识的人,在偶像的庙里吃饭,他的良心若是软弱,他不就放胆去吃那祭过偶像的食物吗?
10Maana, mtu ambaye dhamiri yake ni dhaifu, akikuona wewe mwenye ujuzi unakula vyakula hivyo ndani ya hekalu la sanamu, je, hatatiwa moyo wa kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu?
11因此,基督已经为他死了的那软弱的弟兄,就因你的知识而灭亡了。
11Hivyo, huyo ndugu yako dhaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea kwa sababu ya ujuzi wako.
12你们这样得罪弟兄,伤了他们软弱的良心,就是得罪基督了。
12Kama mkiwakosesha ndugu zenu jinsi hiyo na kuzijeruhi dhamiri zao dhaifu, mtakuwa mmemkosea Kristo.
13所以,如果食物使我的弟兄跌倒,我就永远不再吃肉,免得使我的弟兄跌倒了。
13Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi.