1马其顿圣徒乐捐的榜样
1Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
2他们在患难中受到极大的考验的时候,他们满溢的喜乐和极度的贫乏,汇流出丰厚的慷慨来。
2Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
3我可以作证,他们是按着能力,并且是超过了能力,
3Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
4自动地再三恳求我们,准许他们在供应圣徒的事上有分。
4walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
5他们超过了我们所期望的,照着 神的旨意,先把自己献给主,然后献给我们。
5Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6因此,我们勉励提多,既然开始了这慈善的事,就应当在你们那里把这事办好。
6Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
7你们在一切事上,就如信心、口才、知识、热情和爱我们的心,既然都是富足的,那么,在这慈善的事上,也要显出你们是富足的。
7Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
8劝信徒完成慈善的事我这样说,不是吩咐你们,而是借着别人的热心来考验你们的爱心是否真实。
8Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
9你们是知道我们的主耶稣基督的恩典的:他本来富足,却为你们成了贫穷,要使你们因他的贫穷成为富足。
9Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
10我在这里表示我的意见,这对你们是有益的:你们不仅一年前就在办这事,而且早就想这样作了,
10Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
11现在就应当把这事办好;这样,你们既然有愿意作的心,因着你们尽了自己所能的,就可以完成。
11Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
12因为人要是有愿意作的心,按照他所有的,必蒙悦纳,不是按照他所没有的。
12Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
13这不是要别人轻省,你们受累,而是要大家都均等。
13Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
14现在你们富裕,就要补助他们的缺乏,到了他们富裕的时候,也可以补助你们的缺乏,这样就均等了;
14Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
15正如经上所记:“多的,没有剩余,少的,也不缺乏。”
15Kama Maandiko yasemavyo: "Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa."
16感谢 神,他把我对你们那样的热情,放在提多的心里。
16Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
17提多一方面接受了劝勉,但他自己更加热心,自愿到你们那里去。
17Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
18我们还派了一位弟兄和他同去,(这人在福音的事工上,得到了众教会的称赞。
18Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
19不但这样,众教会更选派了他作我们的旅伴。我们办理这慈善的事,是为了主的荣耀,也是为了我们的心愿。)
19Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
20免得有人因为我们经管的捐款太多,就毁谤我们。
20Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
21因为我们努力去作的,不仅是主认为是美的事,也是众人认为是美的事。
21Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
22我们还派了另一位弟兄与他们同去;我们在许多的事上多次考验过他,知道他很热心;现在他对你们大有信心,就更加热心了。
22Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
23至于提多,他是我的同伴,为你们的缘故作了我的同工;还有我们那两位弟兄,他们是众教会所派的,是基督的荣耀。
23Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
24所以,你们要在众教会面前,向他们证明你们的爱心和我们所夸耀你们的。
24Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.