聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

8

1扫罗迫害教会
1Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
2有些虔诚的人安葬了司提反,为他大大悲痛一番。
2Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
3扫罗却残害教会,逐家进去,连男带女拉去坐监。
3Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
4福音传到撒玛利亚那些分散的人,经过各地,传扬福音真道。
4Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
5腓利下到撒玛利亚城,宣讲基督。
5Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
6群众听了腓利所讲的,看见他所行的神迹,就同心听从了他的话。
6Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
7许多人有污灵附在他们身上,污灵大声喊叫了之后,就出来了;还有许多瘫子瘸子都医好了。
7Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
8在那城里,就大有欢乐。
8Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
9有一个人名叫西门,从前在城里行过邪术,使撒玛利亚的居民惊奇,他又自命不凡,
9Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
10城里大大小小都听从他,说:“这就是那称为‘ 神的大能’的人。”
10Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, "Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa."
11他们听从他,因为他长久用邪术,使他们惊奇。
11Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
12等到腓利向他们传了 神的国的福音,和耶稣基督的名,他们就信了腓利,连男带女都受了洗。
12Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
13连西门自己也信了,他受洗之后,常和腓利在一起,看见所发生的神迹和大能的事,就觉得很惊奇。
13Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
14在耶路撒冷的使徒,听见撒玛利亚居民领受了 神的道,就差派彼得和约翰到他们那里去。
14Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
15二人到了,就为大家祷告,要让他们接受圣灵。
15Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
16因为圣灵还没有降在他们任何一个身上,他们只是受了洗归入主耶稣的名下。
16maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
17于是使徒为他们按手,他们就受了圣灵。
17Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
18西门看见使徒一按手,就有圣灵赐下来,就拿钱给他们,
18Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
19说:“请把这权柄也给我,叫我为谁按手,谁就可以受圣灵。”
19"Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu."
20彼得对他说:“你的银子跟你一同灭亡吧!因为你以为 神的恩赐,是可以用钱买的。
20Lakini Petro akamjibu, "Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
21你和这件事是毫无关系的,因为你在 神面前存心不正。
21Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
22所以,你要悔改离弃这罪恶,要祈求主,也许你心中的意念可以得到赦免。
22Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
23我看出你正在苦胆之中,邪恶捆绑着你。”
23Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!"
24西门回答:“请你们为我求主,好让你们所说的,没有一样临到我身上。”
24Simoni akajibu, "Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema."
25使徒作了见证,讲了主的道,就回耶路撒冷去,一路上在撒玛利亚人的许多村庄里传扬福音。
25Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
26腓利对太监传讲耶稣有主的一位使者对腓利说:“起来,向南走,往那从耶路撒冷下迦萨的路上去。”那条路在旷野里。
26Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, "Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza." (Njia hiyo hupita jangwani.)
27他就动身去了。有一个衣索匹亚人,是衣索匹亚女王干大基有权力的太监,掌管女王全部国库。他上耶路撒冷去礼拜。
27Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
28他回去的时候,坐在车上读以赛亚先知的书。
28Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
29圣灵对腓利说:“你往前去,靠近那车子!”
29Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, "Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo."
30腓利就跑过去,听见他读以赛亚先知的书,就问他:“你所读的,你明白吗?”
30Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, "Je, unaelewa hayo unayosoma?"
31他说:“没有人指导我,怎能明白呢?”于是请腓利上车,同他坐在一起。
31Huyo mtu akamjibu, "Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?" Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
32他所读的那段经文,就是:“他像羊被牵去宰杀,又像羊羔在剪毛的人面前无声,他总是这样不开口。
32Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: "Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
33他受屈辱的时候,得不到公平的审判,谁能说出他的身世呢?因为他的生命从地上被夺去。”
33Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani."
34太监对腓利说:“请问先知这话是指谁说的?指他自己呢?还是指别人?”
34Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, "Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?"
35腓利就开口,从这段经文开始,向他传讲耶稣。
35Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
36他们一路走,到了有水的地方,太监说:“你看,这里有水,有什么可以阻止我受洗呢?”
36Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, "Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?"
37(有些抄本在此有第37节:“腓利说:‘你若全心相信,就可以受洗。’他回答说:‘我信耶稣基督是 神的儿子。’”)
37Filipo akasema, "Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa." Naye akajibu, "Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu."
38于是太监吩咐停车,腓利和他两人下到水中,腓利就给他施洗。
38Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
39他们从水里上来的时候,主的灵就把腓利提去了,太监再也看不见他,就欢欢喜喜地上路。
39Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
40后来有人在亚锁都遇见腓利。他走遍各城,传讲福音,直到该撒利亚。
40Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.