聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Hebrews

10

1律法既然是以后要来的美好事物的影子,不是本体的真象,就不能凭着每年献同样的祭品,使那些进前来的人得到完全。
1Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2如果敬拜的人一次得洁净,良心就不再觉得有罪,那么,献祭的事不是早就停止了吗?
2Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3可是那些祭品,却使人每年都想起罪来,
3Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4因为公牛和山羊的血不能把罪除去。
4Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5所以,基督到世上来的时候,就说:“祭品和礼物不是你所要的,你却为我预备了身体。
5Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: "Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6燔祭和赎罪祭,不是你所喜悦的;
6Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7那时我说:‘看哪!我来了,经卷上已经记载我的事, 神啊!我来是要遵行你的旨意。’”
7Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria."
8前面说:“祭品和礼物,燔祭和赎罪祭,不是你所要的,也不是你所喜悦的。”这些都是按照律法献的;
8Kwanza alisema: "Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi." Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9接着又说:“看哪!我来了,是要遵行你的旨意。”可见他废除那先前的,为要建立那后来的。
9Kisha akasema: "Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako." Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10我们凭着这旨意,借着耶稣基督一次献上他的身体,就已经成圣。
10Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11所有的祭司都是天天站着事奉,多次献上同样的祭品,那些祭品永远不能把罪除去。
11Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12唯有基督献上了一次永远有效的赎罪祭,就在 神的右边坐下来。
12Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13此后,只是等待 神把他的仇敌放在他的脚下,作他的脚凳。
13Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14因为他献上了一次的祭,就使那些成圣的人永远得到完全。
14Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15圣灵也向我们作见证,因为后来他说过:
15Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16“主说:‘在那些日子以后,我要与他们所立的约是这样:我要把我的律法放在他们的心思里面,写在他们的心上。’”
16"Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao."
17又说:“我决不再记着他们的罪恶,和不法的行为。”
17Kisha akaongeza kusema: "Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu."
18这一切既然都赦免了,就不必再为罪献祭了。
18Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19劝勉和警告所以,弟兄们!我们凭着耶稣的血,可以坦然无惧地进入至圣所。
19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20这进入的路,是他给我们开辟的,是一条通过幔子、又新又活的路,这幔子就是他的身体。
20Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21我们既然有一位伟大的祭司治理 神的家,
21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22我们良心的邪恶既然被洒净,身体也用清水洗净了,那么,我们就应该怀着真诚的心和完备的信,进到 神面前;
22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23又应该坚持我们所宣认的盼望,毫不动摇,因为那应许我们的是信实的。
23Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24我们又应该彼此关心,激发爱心,勉励行善。
24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25我们不可放弃聚会,好像有些人的习惯一样;却要互相劝勉。你们既然知道那日子临近,就更应该这样。
25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26如果我们领受了真理的知识以后,还是故意犯罪,就再没有留下赎罪的祭品了;
26Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27只好恐惧地等待着审判,和那快要吞灭众仇敌的烈火。
27Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28如果有人干犯了摩西的律法,凭着两三个证人,他尚且得不到怜悯而死;
28Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29何况是践踏 神的儿子,把那使他成圣的立约的血当作俗物,又侮辱施恩的圣灵的人,你们想想,他不是应该受更严厉的刑罚吗?
29Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30因为我们知道谁说过:“伸冤在我,我必报应。”又说:“主必定审判他自己的子民。”
30Maana tunamfahamu yule aliyesema, "Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza," na ambaye alisema pia, "Bwana atawahukumu watu wake."
31落在永活的 神手里,真是可怕的。
31Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32要忍耐行完 神的旨意你们要回想从前的日子,那时,你们蒙了光照,忍受了许多痛苦的煎熬;
32Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33有时在众人面前被辱骂,遭患难;有时却成了遭遇同样情形的人的同伴。
33Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34你们同情那些遭监禁的人;你们的家业被抢夺的时候,又以喜乐的心接受,因为知道自己有更美长存的家业。
34Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35所以,你们不可丢弃坦然无惧的心,这样的心是带有大赏赐的。
35Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36你们还需要忍耐,好使你们行完了 神的旨意,可以领受所应许的。
36Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37因为:“还有一点点的时候,那要来的就来,并不迟延。
37Maana kama yasemavyo Maandiko: "Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38我的义人必因信得生,如果他后退,我的心就不喜悦他。”
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye."
39但我们不是那些后退以致灭亡的人,而是有信心以致保全生命的人。
39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.