1耶稣复活(太28:1-8;可16:1-8;约20:1-10)
1Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
2发现石头已经从坟墓辊开了,
2Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
3就进去,却找不着主耶稣的身体。
3Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
4她们正为此事猜疑的时候,忽然有两个人,穿着闪烁耀目的衣服,站在她们旁边。
4Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
5她们害怕,把脸伏在地上。那两个人对她们说:“为什么在死人中找活人呢?
5Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, "Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
6他不在这里,已经复活了。你们应当记得他还在加利利的时候,怎样告诉你们,
6Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
7说:‘人子必须被交在罪人手里,钉在十字架上,第三日复活。’”
7Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka."
8她们就想起他的话,
8Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
9于是从坟地回去,把这一切事告诉十一个使徒和其余的人。
9wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
10那些妇女就是抹大拉的马利亚,约亚拿和雅各的母亲马利亚,以及其他在一起的妇女,她们把这些事向使徒说了。
10Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
11使徒以为这些话是无稽之谈,就不相信。
11Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
12彼得却起来跑到坟墓那里,屈身往里观看,只见细麻布在那里,就回去了,对所发生的事非常惊奇。
12Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
13在以马午斯路上显现(可16:12-13)同一天,门徒中有两个人往一个叫以马午斯的村子去,那村子距耶路撒冷约十一公里;
13Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
14他们彼此谈论所发生的这一切事。
14Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
15正在交谈议论的时候,耶稣亲自走近他们,与他们同行,
15Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
16但他们的眼睛却给蒙蔽了,认不出他来。
16Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
17耶稣说:“你们走路的时候,彼此讨论的是什么事呢?”他们就站住,面带愁容;
17Akawauliza, "Mnazungumza nini huku mnatembea?" Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
18一个名叫革流巴的回答他:“在耶路撒冷作客的,难道只有你不知道这几天在那里所发生的事吗?”
18Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, "Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?"
19他说:“什么事呢?”他们说:“就是拿撒勒人耶稣的事。他是先知,在 神和众人面前,说话行事都有大能。
19Naye akawajibu, "Mambo gani?" Wao wakamjibu, "Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
20我们的祭司长和官长,竟把他交出去,判了死罪,钉在十字架上。
20Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
21但我们素来盼望要救赎以色列的就是他。不但这样,这些事发生到今天,已经是第三天了。
21Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
22而且我们中间有几个妇女使我们惊奇,她们清早到坟墓那里去,
22Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
23却找不到他的身体。她们回来说看见天使显现,天使说他活了。
23wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
24又有我们中间的几个人到坟墓那里去,所看见的正如妇女们所说的,只是没有看见他。”
24Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona."
25耶稣说:“无知的人哪,先知所说的一切话,你们心里信得太迟钝了!
25Kisha Yesu akawaambia, "Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
26基督这样受害,然后进入他的荣耀,不是应当的吗?”
26Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?"
27于是他从摩西和众先知起,把所有关于自己的经文,都给他们解释明白了。
27Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
28他们走近要去的村子,他好像还要往前行,
28Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
29他们强留他说:“天晚了,太阳下山了,请与我们同住吧!”他就进去与他们同住。
29lakini wao wakamsihi wakisema, "Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia." Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
30到了吃饭的时候,他拿起饼来,感谢了,擘开递给他们,
30Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
31他们的眼睛开了,才认出是耶稣来;他却从他们面前不见了。
31Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
32他们彼此说:“在路上他对我们说话,给我们解释圣经的时候,我们的心不是火热的吗?”
32Basi, wakaambiana, "Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?"
33他们就立时起来回耶路撒冷去。在那里遇见十一个使徒和跟他们聚在一起的人,
33Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34说:“主果然复活了,已经向西门显现了。”
34wakisema, "Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni."
35两个人就把在路上的事,和擘饼的时候他们怎样认出耶稣来的事,都述说了一遍。
35Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
36向众门徒显现(太28:16-20;可16:14-18;约20:19-23。参徒1:6-8)正说这话的时候,耶稣亲自站在他们当中,说:“愿你们平安。”
36Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia "Amani kwenu."
37他们非常惊怕,以为看见了灵。
37Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
38他说:“你们为什么惊慌,为什么心里疑惑呢?
38Lakini yeye akawaambia, "Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
39你们看我的手、我的脚,就知道我是谁。摸我看看,灵没有骨,没有肉;你们看,我是有的。”
39Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo."
40说了这话,就把手和脚给他们看。
40Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
41他们欢喜到不敢相信,并且很惊奇。耶稣说:“你们这里有什么吃的没有?”
41Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, "Mnacho chakula chochote hapa?"
42他们就给了他一片烧鱼。
42Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
43他接过来,在他们面前吃了。
43Akakichukua, akala, wote wakimwona.
44主对他们说:“这就是我从前与你们同在的时候,对你们说过的话:摩西的律法、先知书和诗篇上所记关于我的一切事,都必定应验。”
44Halafu akawaambia, "Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi."
45于是他开他们的心窍,使他们明白圣经;
45Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
46又说:“经上这样记着:基督必须受害,第三天从死人中复活。
46Akawaambia, "Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
47人要奉他的名,传讲悔改与赦罪的道,从耶路撒冷起,直传到万国。
47na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
48你们就是这些事的见证。
48Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
49我要使我父的应许临到你们身上,你们当在城里等候,直到得着从上面来的能力。”
49Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu."
50耶稣升天(参可16:19-20;徒1:9-11)主带他们出去,到了伯大尼附近,举手给他们祝福。
50Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
51正在祝福的时候,他就离开他们,被接到天上去了。
51Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
52他们就敬拜他,欢欢喜喜地回到耶路撒冷,
52Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
53常常在殿里称颂 神。
53wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.