聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

12

1献上自己当作活祭
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2不要模仿这个世代,倒要借着心意的更新而改变过来,使你们可以察验出什么是 神的旨意,就是察验出什么是美好的、蒙他悦纳的和完全的事。
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3信徒行事为人的准则我凭着所赐给我的恩典,对你们各人说,不可自视太高,高于所当看的,反而应该照着 神分给各人信心的大小,看得适中。
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4就像一个身体有许多肢体,各肢体都有不同的功用;
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5照样,我们大家在基督里成为一个身体,也是互相作肢体。
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6照着所赐给我们的恩典,我们各有不同的恩赐:说预言的,就应当照着信心的程度去说;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7服事人的,就应当照着恩赐去服事;教导的,就应当照着恩赐教导;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8劝慰的,就应当照着恩赐劝慰;把财物分给人的要真诚;领导的要殷勤;行善的要乐意。
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9爱,不可虚伪;恶,要厌恶;善,要持守。
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10要以手足之爱彼此相亲,用恭敬的心互相礼让。
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11殷勤不可懒惰,心灵要火热,常常服事主;
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12在盼望中要喜乐,在患难中要坚忍,祷告要恒切。
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13圣徒有缺乏的,就要接济;客旅要热诚地款待。
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14迫害你们的,要为他们祝福;只可祝福,不可咒诅。
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15要与喜乐的人一同喜乐,与哀哭的人一同哀哭。
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16要彼此同心,不可心高气傲,倒要俯就卑微的。不可自以为聪明。
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17不可以恶报恶。大家以为美的事,要努力去作。
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18可能的话,总要尽你们的所能与人和睦。
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19亲爱的啊,不要为自己伸冤,宁可等候主的忿怒,因为经上记着,主说:“伸冤在我,我必报应。”
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20相反地,“如果你的仇敌饿了,就给他吃;如果渴了,就给他喝。因为你这样作,就是把炭火堆在他的头上。”
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21不可被恶所胜,反要以善胜恶。
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.