聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

5

1因信称义后所得的恩典
1Sasa, kwa vile tumekubaliwa kuwa wadilifu kwa imani, basi, tunayo amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo.
2我们也凭着信,借着他可以进入现在所站的这恩典中,并且以盼望得享 神的荣耀为荣。
2Kwa imani yetu, yeye ametuleta katika hali hii ya neema ya Mungu ambamo sasa tunaishi. Basi, tunajivunia tumaini tulilo nalo la kushiriki utukufu wa Mungu.
3不但这样,我们更以患难为荣;知道患难产生忍耐,
3Naam, si hayo tu, bali tunafurahi pia katika taabu tukijua kwamba taabu huleta saburi,
4忍耐产生毅力,毅力产生盼望;
4nayo saburi huleta uthabiti, na uthabiti huleta tumaini.
5盼望是不会令人蒙羞的,因为 神借着所赐给我们的圣灵,把他的爱浇灌在我们的心里。
5Tumaini hilo haliwezi kutuhadaa, maana Mungu amekwisha miminia mioyoni mwetu upendo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu aliyetujalia.
6当我们还软弱的时候,基督就照所定的日期,为不敬虔的人死了。
6Tulipokuwa bado wanyonge, Kristo, wakati ulipotimia, alikufa kwa ajili yetu sisi waovu.
7为义人死,是少有的;为好人死,或有敢作的;
7Si rahisi mtu kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; labda mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
8唯有基督在我们还作罪人的时候为我们死, 神对我们的爱就在此显明了。
8Lakini Mungu amethibitisha kwamba anatupenda, maana wakati tulipokuwa bado wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
9所以,我们现在既然因他的血称义,就更要借着他免受 神的忿怒。
9Kwa kuwa sasa tumekubaliwa kuwa waadilifu kwa damu ya Kristo, ni dhahiri zaidi kwamba atatuokoa katika ghadhabu ya Mungu.
10我们作仇敌的时候,尚且借着 神儿子的死与他复和,既然复和了,就更要因他的生得救了!
10Maana, tulipokuwa bado adui zake, Mungu alitupatanisha naye kwa kifo cha Mwanae. Na kwa vile sasa tumepatanishwa naye, ni dhahiri zaidi kwamba tutaokolewa kwa uzima wa Kristo.
11不但这样,我们现在已经借着我们的主耶稣基督与 神复和,也借着他以 神为荣。
11Wala si hayo tu, ila tunafurahi pia katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ametupatanisha na Mungu.
12亚当与基督的比较正好像罪借着一个人入了世界,死又是从罪来的,所以死就临到全人类,因为人人都犯了罪。
12Kwa njia ya mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, nayo ikasababisha kifo. Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu, kwa maana wote wametenda dhambi.
13没有律法以前,罪已经在世界上了;不过,没有律法的时候,罪也不算罪。
13Kabla ya Sheria kuwako, dhambi ilikuwako ulimwenguni; lakini dhambi haiwekwi katika kumbukumbu bila sheria.
14可是,从亚当到摩西,死就掌权了,甚至那些不像亚当那样犯罪的人,也在死的权下;亚当正是要来的那一位的预表。
14Lakini tangu wakati wa Adamu mpaka wakati wa Mose, kifo kiliwatawala hata wale ambao hawakutenda dhambi kama ile ya Adamu, ya kumwasi Mungu. Adamu alikuwa kielelezo cha yule ambaye atakuja baadaye.
15但恩赏和过犯是截然不同的;如果因着那一人的过犯,众人都死了, 神的恩典和这一人耶稣基督在恩典里的赏赐,对众人就更加丰盛了。
15Lakini ipo tofauti: neema ya Mungu si kama dhambi ya Adamu. Maana, ingawa dhambi ya mtu mmoja ilisababisha kifo kwa wote, kwa fadhili ya mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, Mungu amewazidishia wote neema na zawadi zake.
16这赏赐和那一人犯罪的后果也是不同的;因为审判是由一人而来,以致定罪,恩赏却由许多过犯而来,以致称义。
16Kuna tofauti baina ya zawadi ya Mungu, na dhambi ya mtu yule mmoja. Maana, baada ya kosa la mtu mmoja, Mungu alitoa hukumu; lakini baada ya makosa ya watu wengi, Mungu aliwapa zawadi yake kwa kuwasamehe.
17如果因着那一人的过犯,死就因那一人而掌权,那些蒙丰富的恩典并且得公义为赏赐的,就更要因这一位耶稣基督在生命中掌权了。
17Kweli, kwa dhambi ya mtu mmoja kifo kilianza kutawala kwa sababu ya huyo mtu mmoja; lakini, ni dhahiri zaidi kwamba alichokifanya yule mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, ni bora zaidi. Wote wanaopokea neema na zawadi hiyo ya kukubaliwa kuwa waadilifu, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mmoja, yaani Yesu Kristo.
18这样看来,因一次的过犯,全人类都被定罪;照样,因一次的义行,全人类都被称义得生命了。
18Basi, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta hukumu kwa binadamu wote, kadhalika kitendo kimoja kiadilifu kinawapa uhuru na uzima.
19因着那一人的悖逆,众人就被列为罪人;照样,因着这一人的顺服,众人也被列为义人了。
19Na kama kwa kutotii kwa mtu mmoja watu wengi walifanywa wenye dhambi, kadhalika kutii kwa mtu mmoja kutawafanya wengi wakubaliwe kuwa waadilifu.
20律法的出现,是要叫过犯增多;然而罪在哪里增多,恩典就更加增多了。
20Sheria ilitokea, ikasababisha kuongezeka kwa uhalifu; lakini pale dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi.
21罪借着死掌权;照样,恩典也借着义掌权,使人借着我们的主耶稣基督进入永生。
21Kama vile dhambi ilivyotawala kwa kifo, kadhalika neema inatawala kwa njia ya uadilifu, na kuleta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.