King James Version

Swahili: New Testament

1 Thessalonians

5

1But of the times and the seasons, brethren, ye have no need that I write unto you.
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2For yourselves know perfectly that the day of the Lord so cometh as a thief in the night.
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3For when they shall say, Peace and safety; then sudden destruction cometh upon them, as travail upon a woman with child; and they shall not escape.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4But ye, brethren, are not in darkness, that that day should overtake you as a thief.
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5Ye are all the children of light, and the children of the day: we are not of the night, nor of darkness.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6Therefore let us not sleep, as do others; but let us watch and be sober.
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7For they that sleep sleep in the night; and they that be drunken are drunken in the night.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8But let us, who are of the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love; and for an helmet, the hope of salvation.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9For God hath not appointed us to wrath, but to obtain salvation by our Lord Jesus Christ,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10Who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11Wherefore comfort yourselves together, and edify one another, even as also ye do.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12And we beseech you, brethren, to know them which labour among you, and are over you in the Lord, and admonish you;
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13And to esteem them very highly in love for their work's sake. And be at peace among yourselves.
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14Now we exhort you, brethren, warn them that are unruly, comfort the feebleminded, support the weak, be patient toward all men.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15See that none render evil for evil unto any man; but ever follow that which is good, both among yourselves, and to all men.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16Rejoice evermore.
16Furahini daima,
17Pray without ceasing.
17salini kila wakati
18In every thing give thanks: for this is the will of God in Christ Jesus concerning you.
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19Quench not the Spirit.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20Despise not prophesyings.
20msidharau unabii.
21Prove all things; hold fast that which is good.
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22Abstain from all appearance of evil.
22na epukeni kila aina ya uovu.
23And the very God of peace sanctify you wholly; and I pray God your whole spirit and soul and body be preserved blameless unto the coming of our Lord Jesus Christ.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24Faithful is he that calleth you, who also will do it.
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25Brethren, pray for us.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26Greet all the brethren with an holy kiss.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27I charge you by the Lord that this epistle be read unto all the holy brethren.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.