1I exhort therefore, that, first of all, supplications, prayers, intercessions, and giving of thanks, be made for all men;
1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2For kings, and for all that are in authority; that we may lead a quiet and peaceable life in all godliness and honesty.
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3For this is good and acceptable in the sight of God our Saviour;
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4Who will have all men to be saved, and to come unto the knowledge of the truth.
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5For there is one God, and one mediator between God and men, the man Christ Jesus;
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6Who gave himself a ransom for all, to be testified in due time.
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7Whereunto I am ordained a preacher, and an apostle, (I speak the truth in Christ, and lie not;) a teacher of the Gentiles in faith and verity.
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8I will therefore that men pray every where, lifting up holy hands, without wrath and doubting.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9In like manner also, that women adorn themselves in modest apparel, with shamefacedness and sobriety; not with broided hair, or gold, or pearls, or costly array;
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10But (which becometh women professing godliness) with good works.
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11Let the woman learn in silence with all subjection.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12But I suffer not a woman to teach, nor to usurp authority over the man, but to be in silence.
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13For Adam was first formed, then Eve.
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14And Adam was not deceived, but the woman being deceived was in the transgression.
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15Notwithstanding she shall be saved in childbearing, if they continue in faith and charity and holiness with sobriety.
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.