King James Version

Swahili: New Testament

2 Timothy

4

1I charge thee therefore before God, and the Lord Jesus Christ, who shall judge the quick and the dead at his appearing and his kingdom;
1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2Preach the word; be instant in season, out of season; reprove, rebuke, exhort with all longsuffering and doctrine.
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3For the time will come when they will not endure sound doctrine; but after their own lusts shall they heap to themselves teachers, having itching ears;
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4And they shall turn away their ears from the truth, and shall be turned unto fables.
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5But watch thou in all things, endure afflictions, do the work of an evangelist, make full proof of thy ministry.
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6For I am now ready to be offered, and the time of my departure is at hand.
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7I have fought a good fight, I have finished my course, I have kept the faith:
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8Henceforth there is laid up for me a crown of righteousness, which the Lord, the righteous judge, shall give me at that day: and not to me only, but unto all them also that love his appearing.
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9Do thy diligence to come shortly unto me:
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10For Demas hath forsaken me, having loved this present world, and is departed unto Thessalonica; Crescens to Galatia, Titus unto Dalmatia.
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
11Only Luke is with me. Take Mark, and bring him with thee: for he is profitable to me for the ministry.
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12And Tychicus have I sent to Ephesus.
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13The cloke that I left at Troas with Carpus, when thou comest, bring with thee, and the books, but especially the parchments.
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14Alexander the coppersmith did me much evil: the Lord reward him according to his works:
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15Of whom be thou ware also; for he hath greatly withstood our words.
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16At my first answer no man stood with me, but all men forsook me: I pray God that it may not be laid to their charge.
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17Notwithstanding the Lord stood with me, and strengthened me; that by me the preaching might be fully known, and that all the Gentiles might hear: and I was delivered out of the mouth of the lion.
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18And the Lord shall deliver me from every evil work, and will preserve me unto his heavenly kingdom: to whom be glory for ever and ever. Amen.
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
19Salute Prisca and Aquila, and the household of Onesiphorus.
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20Erastus abode at Corinth: but Trophimus have I left at Miletum sick.
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21Do thy diligence to come before winter. Eubulus greeteth thee, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brethren.
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22The Lord Jesus Christ be with thy spirit. Grace be with you. Amen.
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.