1And the third day there was a marriage in Cana of Galilee; and the mother of Jesus was there:
1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
2And both Jesus was called, and his disciples, to the marriage.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3And when they wanted wine, the mother of Jesus saith unto him, They have no wine.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
4Jesus saith unto her, Woman, what have I to do with thee? mine hour is not yet come.
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
5His mother saith unto the servants, Whatsoever he saith unto you, do it.
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
6And there were set there six waterpots of stone, after the manner of the purifying of the Jews, containing two or three firkins apiece.
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7Jesus saith unto them, Fill the waterpots with water. And they filled them up to the brim.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
8And he saith unto them, Draw out now, and bear unto the governor of the feast. And they bare it.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
9When the ruler of the feast had tasted the water that was made wine, and knew not whence it was: (but the servants which drew the water knew;) the governor of the feast called the bridegroom,
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
10And saith unto him, Every man at the beginning doth set forth good wine; and when men have well drunk, then that which is worse: but thou hast kept the good wine until now.
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
11This beginning of miracles did Jesus in Cana of Galilee, and manifested forth his glory; and his disciples believed on him.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
12After this he went down to Capernaum, he, and his mother, and his brethren, and his disciples: and they continued there not many days.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
13And the Jews' passover was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14And found in the temple those that sold oxen and sheep and doves, and the changers of money sitting:
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
15And when he had made a scourge of small cords, he drove them all out of the temple, and the sheep, and the oxen; and poured out the changers' money, and overthrew the tables;
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
16And said unto them that sold doves, Take these things hence; make not my Father's house an house of merchandise.
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
17And his disciples remembered that it was written, The zeal of thine house hath eaten me up.
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
18Then answered the Jews and said unto him, What sign shewest thou unto us, seeing that thou doest these things?
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
19Jesus answered and said unto them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
20Then said the Jews, Forty and six years was this temple in building, and wilt thou rear it up in three days?
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
21But he spake of the temple of his body.
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
22When therefore he was risen from the dead, his disciples remembered that he had said this unto them; and they believed the scripture, and the word which Jesus had said.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
23Now when he was in Jerusalem at the passover, in the feast day, many believed in his name, when they saw the miracles which he did.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
24But Jesus did not commit himself unto them, because he knew all men,
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
25And needed not that any should testify of man: for he knew what was in man.
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.