King James Version

Swahili: New Testament

Luke

20

1And it came to pass, that on one of those days, as he taught the people in the temple, and preached the gospel, the chief priests and the scribes came upon him with the elders,
1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2And spake unto him, saying, Tell us, by what authority doest thou these things? or who is he that gave thee this authority?
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
3And he answered and said unto them, I will also ask you one thing; and answer me:
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
4The baptism of John, was it from heaven, or of men?
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
5And they reasoned with themselves, saying, If we shall say, From heaven; he will say, Why then believed ye him not?
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6But and if we say, Of men; all the people will stone us: for they be persuaded that John was a prophet.
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
7And they answered, that they could not tell whence it was.
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
8And Jesus said unto them, Neither tell I you by what authority I do these things.
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
9Then began he to speak to the people this parable; A certain man planted a vineyard, and let it forth to husbandmen, and went into a far country for a long time.
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10And at the season he sent a servant to the husbandmen, that they should give him of the fruit of the vineyard: but the husbandmen beat him, and sent him away empty.
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11And again he sent another servant: and they beat him also, and entreated him shamefully, and sent him away empty.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12And again he sent a third: and they wounded him also, and cast him out.
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13Then said the lord of the vineyard, What shall I do? I will send my beloved son: it may be they will reverence him when they see him.
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14But when the husbandmen saw him, they reasoned among themselves, saying, This is the heir: come, let us kill him, that the inheritance may be ours.
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15So they cast him out of the vineyard, and killed him. What therefore shall the lord of the vineyard do unto them?
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16He shall come and destroy these husbandmen, and shall give the vineyard to others. And when they heard it, they said, God forbid.
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
17And he beheld them, and said, What is this then that is written, The stone which the builders rejected, the same is become the head of the corner?
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18Whosoever shall fall upon that stone shall be broken; but on whomsoever it shall fall, it will grind him to powder.
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
19And the chief priests and the scribes the same hour sought to lay hands on him; and they feared the people: for they perceived that he had spoken this parable against them.
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20And they watched him, and sent forth spies, which should feign themselves just men, that they might take hold of his words, that so they might deliver him unto the power and authority of the governor.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21And they asked him, saying, Master, we know that thou sayest and teachest rightly, neither acceptest thou the person of any, but teachest the way of God truly:
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22Is it lawful for us to give tribute unto Caesar, or no?
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
23But he perceived their craftiness, and said unto them, Why tempt ye me?
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24Shew me a penny. Whose image and superscription hath it? They answered and said, Caesar's.
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
25And he said unto them, Render therefore unto Caesar the things which be Caesar's, and unto God the things which be God's.
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
26And they could not take hold of his words before the people: and they marvelled at his answer, and held their peace.
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27Then came to him certain of the Sadducees, which deny that there is any resurrection; and they asked him,
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28Saying, Master, Moses wrote unto us, If any man's brother die, having a wife, and he die without children, that his brother should take his wife, and raise up seed unto his brother.
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29There were therefore seven brethren: and the first took a wife, and died without children.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30And the second took her to wife, and he died childless.
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31And the third took her; and in like manner the seven also: and they left no children, and died.
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
32Last of all the woman died also.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33Therefore in the resurrection whose wife of them is she? for seven had her to wife.
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
34And Jesus answering said unto them, The children of this world marry, and are given in marriage:
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
35But they which shall be accounted worthy to obtain that world, and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage:
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
36Neither can they die any more: for they are equal unto the angels; and are the children of God, being the children of the resurrection.
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37Now that the dead are raised, even Moses shewed at the bush, when he calleth the Lord the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38For he is not a God of the dead, but of the living: for all live unto him.
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
39Then certain of the scribes answering said, Master, thou hast well said.
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
40And after that they durst not ask him any question at all.
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41And he said unto them, How say they that Christ is David's son?
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42And David himself saith in the book of Psalms, The LORD said unto my Lord, Sit thou on my right hand,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43Till I make thine enemies thy footstool.
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44David therefore calleth him Lord, how is he then his son?
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
45Then in the audience of all the people he said unto his disciples,
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46Beware of the scribes, which desire to walk in long robes, and love greetings in the markets, and the highest seats in the synagogues, and the chief rooms at feasts;
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47Which devour widows' houses, and for a shew make long prayers: the same shall receive greater damnation.
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"