1And they came over unto the other side of the sea, into the country of the Gadarenes.
1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2And when he was come out of the ship, immediately there met him out of the tombs a man with an unclean spirit,
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3Who had his dwelling among the tombs; and no man could bind him, no, not with chains:
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4Because that he had been often bound with fetters and chains, and the chains had been plucked asunder by him, and the fetters broken in pieces: neither could any man tame him.
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5And always, night and day, he was in the mountains, and in the tombs, crying, and cutting himself with stones.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6But when he saw Jesus afar off, he ran and worshipped him,
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7And cried with a loud voice, and said, What have I to do with thee, Jesus, thou Son of the most high God? I adjure thee by God, that thou torment me not.
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
8For he said unto him, Come out of the man, thou unclean spirit.
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
9And he asked him, What is thy name? And he answered, saying, My name is Legion: for we are many.
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
10And he besought him much that he would not send them away out of the country.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11Now there was there nigh unto the mountains a great herd of swine feeding.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12And all the devils besought him, saying, Send us into the swine, that we may enter into them.
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
13And forthwith Jesus gave them leave. And the unclean spirits went out, and entered into the swine: and the herd ran violently down a steep place into the sea, (they were about two thousand;) and were choked in the sea.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14And they that fed the swine fled, and told it in the city, and in the country. And they went out to see what it was that was done.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15And they come to Jesus, and see him that was possessed with the devil, and had the legion, sitting, and clothed, and in his right mind: and they were afraid.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16And they that saw it told them how it befell to him that was possessed with the devil, and also concerning the swine.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17And they began to pray him to depart out of their coasts.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18And when he was come into the ship, he that had been possessed with the devil prayed him that he might be with him.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19Howbeit Jesus suffered him not, but saith unto him, Go home to thy friends, and tell them how great things the Lord hath done for thee, and hath had compassion on thee.
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
20And he departed, and began to publish in Decapolis how great things Jesus had done for him: and all men did marvel.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21And when Jesus was passed over again by ship unto the other side, much people gathered unto him: and he was nigh unto the sea.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22And, behold, there cometh one of the rulers of the synagogue, Jairus by name; and when he saw him, he fell at his feet,
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23And besought him greatly, saying, My little daughter lieth at the point of death: I pray thee, come and lay thy hands on her, that she may be healed; and she shall live.
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
24And Jesus went with him; and much people followed him, and thronged him.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25And a certain woman, which had an issue of blood twelve years,
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26And had suffered many things of many physicians, and had spent all that she had, and was nothing bettered, but rather grew worse,
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27When she had heard of Jesus, came in the press behind, and touched his garment.
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28For she said, If I may touch but his clothes, I shall be whole.
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
29And straightway the fountain of her blood was dried up; and she felt in her body that she was healed of that plague.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30And Jesus, immediately knowing in himself that virtue had gone out of him, turned him about in the press, and said, Who touched my clothes?
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
31And his disciples said unto him, Thou seest the multitude thronging thee, and sayest thou, Who touched me?
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
32And he looked round about to see her that had done this thing.
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33But the woman fearing and trembling, knowing what was done in her, came and fell down before him, and told him all the truth.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34And he said unto her, Daughter, thy faith hath made thee whole; go in peace, and be whole of thy plague.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
35While he yet spake, there came from the ruler of the synagogue's house certain which said, Thy daughter is dead: why troublest thou the Master any further?
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
36As soon as Jesus heard the word that was spoken, he saith unto the ruler of the synagogue, Be not afraid, only believe.
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
37And he suffered no man to follow him, save Peter, and James, and John the brother of James.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38And he cometh to the house of the ruler of the synagogue, and seeth the tumult, and them that wept and wailed greatly.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39And when he was come in, he saith unto them, Why make ye this ado, and weep? the damsel is not dead, but sleepeth.
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
40And they laughed him to scorn. But when he had put them all out, he taketh the father and the mother of the damsel, and them that were with him, and entereth in where the damsel was lying.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41And he took the damsel by the hand, and said unto her, Talitha cumi; which is, being interpreted, Damsel, I say unto thee, arise.
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
42And straightway the damsel arose, and walked; for she was of the age of twelve years. And they were astonished with a great astonishment.
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43And he charged them straitly that no man should know it; and commanded that something should be given her to eat.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.