King James Version

Swahili: New Testament

Matthew

20

1For the kingdom of heaven is like unto a man that is an householder, which went out early in the morning to hire labourers into his vineyard.
1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2And when he had agreed with the labourers for a penny a day, he sent them into his vineyard.
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3And he went out about the third hour, and saw others standing idle in the marketplace,
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4And said unto them; Go ye also into the vineyard, and whatsoever is right I will give you. And they went their way.
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5Again he went out about the sixth and ninth hour, and did likewise.
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6And about the eleventh hour he went out, and found others standing idle, and saith unto them, Why stand ye here all the day idle?
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7They say unto him, Because no man hath hired us. He saith unto them, Go ye also into the vineyard; and whatsoever is right, that shall ye receive.
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8So when even was come, the lord of the vineyard saith unto his steward, Call the labourers, and give them their hire, beginning from the last unto the first.
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9And when they came that were hired about the eleventh hour, they received every man a penny.
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10But when the first came, they supposed that they should have received more; and they likewise received every man a penny.
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11And when they had received it, they murmured against the goodman of the house,
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12Saying, These last have wrought but one hour, and thou hast made them equal unto us, which have borne the burden and heat of the day.
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13But he answered one of them, and said, Friend, I do thee no wrong: didst not thou agree with me for a penny?
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14Take that thine is, and go thy way: I will give unto this last, even as unto thee.
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15Is it not lawful for me to do what I will with mine own? Is thine eye evil, because I am good?
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
16So the last shall be first, and the first last: for many be called, but few chosen.
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
17And Jesus going up to Jerusalem took the twelve disciples apart in the way, and said unto them,
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18Behold, we go up to Jerusalem; and the Son of man shall be betrayed unto the chief priests and unto the scribes, and they shall condemn him to death,
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19And shall deliver him to the Gentiles to mock, and to scourge, and to crucify him: and the third day he shall rise again.
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
20Then came to him the mother of Zebedees children with her sons, worshipping him, and desiring a certain thing of him.
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21And he said unto her, What wilt thou? She saith unto him, Grant that these my two sons may sit, the one on thy right hand, and the other on the left, in thy kingdom.
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
22But Jesus answered and said, Ye know not what ye ask. Are ye able to drink of the cup that I shall drink of, and to be baptized with the baptism that I am baptized with? They say unto him, We are able.
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
23And he saith unto them, Ye shall drink indeed of my cup, and be baptized with the baptism that I am baptized with: but to sit on my right hand, and on my left, is not mine to give, but it shall be given to them for whom it is prepared of my Father.
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
24And when the ten heard it, they were moved with indignation against the two brethren.
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25But Jesus called them unto him, and said, Ye know that the princes of the Gentiles exercise dominion over them, and they that are great exercise authority upon them.
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26But it shall not be so among you: but whosoever will be great among you, let him be your minister;
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27And whosoever will be chief among you, let him be your servant:
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28Even as the Son of man came not to be ministered unto, but to minister, and to give his life a ransom for many.
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
29And as they departed from Jericho, a great multitude followed him.
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30And, behold, two blind men sitting by the way side, when they heard that Jesus passed by, cried out, saying, Have mercy on us, O Lord, thou son of David.
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31And the multitude rebuked them, because they should hold their peace: but they cried the more, saying, Have mercy on us, O Lord, thou son of David.
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
32And Jesus stood still, and called them, and said, What will ye that I shall do unto you?
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
33They say unto him, Lord, that our eyes may be opened.
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
34So Jesus had compassion on them, and touched their eyes: and immediately their eyes received sight, and they followed him.
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.