King James Version

Swahili: New Testament

Romans

12

1I beseech you therefore, brethren, by the mercies of God, that ye present your bodies a living sacrifice, holy, acceptable unto God, which is your reasonable service.
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2And be not conformed to this world: but be ye transformed by the renewing of your mind, that ye may prove what is that good, and acceptable, and perfect, will of God.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3For I say, through the grace given unto me, to every man that is among you, not to think of himself more highly than he ought to think; but to think soberly, according as God hath dealt to every man the measure of faith.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4For as we have many members in one body, and all members have not the same office:
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5So we, being many, are one body in Christ, and every one members one of another.
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6Having then gifts differing according to the grace that is given to us, whether prophecy, let us prophesy according to the proportion of faith;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7Or ministry, let us wait on our ministering: or he that teacheth, on teaching;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8Or he that exhorteth, on exhortation: he that giveth, let him do it with simplicity; he that ruleth, with diligence; he that sheweth mercy, with cheerfulness.
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9Let love be without dissimulation. Abhor that which is evil; cleave to that which is good.
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10Be kindly affectioned one to another with brotherly love; in honour preferring one another;
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11Not slothful in business; fervent in spirit; serving the Lord;
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12Rejoicing in hope; patient in tribulation; continuing instant in prayer;
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13Distributing to the necessity of saints; given to hospitality.
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14Bless them which persecute you: bless, and curse not.
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15Rejoice with them that do rejoice, and weep with them that weep.
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16Be of the same mind one toward another. Mind not high things, but condescend to men of low estate. Be not wise in your own conceits.
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17Recompense to no man evil for evil. Provide things honest in the sight of all men.
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18If it be possible, as much as lieth in you, live peaceably with all men.
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19Dearly beloved, avenge not yourselves, but rather give place unto wrath: for it is written, Vengeance is mine; I will repay, saith the Lord.
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20Therefore if thine enemy hunger, feed him; if he thirst, give him drink: for in so doing thou shalt heap coals of fire on his head.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21Be not overcome of evil, but overcome evil with good.
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.