1What advantage then hath the Jew? or what profit is there of circumcision?
1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
2Much every way: chiefly, because that unto them were committed the oracles of God.
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
3For what if some did not believe? shall their unbelief make the faith of God without effect?
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
4God forbid: yea, let God be true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy sayings, and mightest overcome when thou art judged.
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
5But if our unrighteousness commend the righteousness of God, what shall we say? Is God unrighteous who taketh vengeance? (I speak as a man)
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
6God forbid: for then how shall God judge the world?
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
7For if the truth of God hath more abounded through my lie unto his glory; why yet am I also judged as a sinner?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
8And not rather, (as we be slanderously reported, and as some affirm that we say,) Let us do evil, that good may come? whose damnation is just.
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
9What then? are we better than they? No, in no wise: for we have before proved both Jews and Gentiles, that they are all under sin;
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
10As it is written, There is none righteous, no, not one:
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
11There is none that understandeth, there is none that seeketh after God.
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12They are all gone out of the way, they are together become unprofitable; there is none that doeth good, no, not one.
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13Their throat is an open sepulchre; with their tongues they have used deceit; the poison of asps is under their lips:
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14Whose mouth is full of cursing and bitterness:
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15Their feet are swift to shed blood:
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16Destruction and misery are in their ways:
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17And the way of peace have they not known:
17njia ya amani hawaijui.
18There is no fear of God before their eyes.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
19Now we know that what things soever the law saith, it saith to them who are under the law: that every mouth may be stopped, and all the world may become guilty before God.
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
20Therefore by the deeds of the law there shall no flesh be justified in his sight: for by the law is the knowledge of sin.
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
21But now the righteousness of God without the law is manifested, being witnessed by the law and the prophets;
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
22Even the righteousness of God which is by faith of Jesus Christ unto all and upon all them that believe: for there is no difference:
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
23For all have sinned, and come short of the glory of God;
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
24Being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
25Whom God hath set forth to be a propitiation through faith in his blood, to declare his righteousness for the remission of sins that are past, through the forbearance of God;
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
26To declare, I say, at this time his righteousness: that he might be just, and the justifier of him which believeth in Jesus.
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
27Where is boasting then? It is excluded. By what law? of works? Nay: but by the law of faith.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
28Therefore we conclude that a man is justified by faith without the deeds of the law.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
29Is he the God of the Jews only? is he not also of the Gentiles? Yes, of the Gentiles also:
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
30Seeing it is one God, which shall justify the circumcision by faith, and uncircumcision through faith.
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
31Do we then make void the law through faith? God forbid: yea, we establish the law.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.