1And concerning the collection that [is] for the saints, as I directed to the assemblies of Galatia, so also ye — do ye;
1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2on every first [day] of the week, let each one of you lay by him, treasuring up whatever he may have prospered, that when I may come then collections may not be made;
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3and whenever I may come, whomsoever ye may approve, through letters, these I will send to carry your favour to Jerusalem;
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4and if it be meet for me also to go, with me they shall go.
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5And I will come unto you, when I pass through Macedonia — for Macedonia I do pass through —
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
6and with you, it may be, I will abide, or even winter, that ye may send me forward whithersoever I go,
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7for I do not wish to see you now in the passing, but I hope to remain a certain time with you, if the Lord may permit;
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8and I will remain in Ephesus till the Pentecost,
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9for a door to me hath been opened — great and effectual — and withstanders [are] many.
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10And if Timotheus may come, see that he may become without fear with you, for the work of the Lord he doth work, even as I,
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11no one, then, may despise him; and send ye him forward in peace, that he may come to me, for I expect him with the brethren;
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12and concerning Apollos our brother, much I did entreat him that he may come unto you with the brethren, and it was not at all [his] will that he may come now, and he will come when he may find convenient.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13Watch ye, stand in the faith; be men, be strong;
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14let all your things be done in love.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15And I entreat you, brethren, ye have known the household of Stephanas, that it is the first-fruit of Achaia, and to the ministration to the saints they did set themselves —
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16that ye also be subject to such, and to every one who is working with [us] and labouring;
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17and I rejoice over the presence of Stephanas, and Fortunatus, and Achaicus, because the lack of you did these fill up;
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18for they did refresh my spirit and yours; acknowledge ye, therefore, those who [are] such.
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19Salute you do the assemblies of Asia; salute you much in the Lord do Aquilas and Priscilla, with the assembly in their house;
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20salute you do all the brethren; salute ye one another in an holy kiss.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21The salutation of [me] Paul with my hand;
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22if any one doth not love the Lord Jesus Christ — let him be anathema! The Lord hath come!
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
23The grace of the Lord Jesus Christ [is] with you;
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24my love [is] with you all in Christ Jesus. Amen.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.