Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

1 Peter

4

1Christ, then, having suffered for us in the flesh, ye also with the same mind arm yourselves, because he who did suffer in the flesh hath done with sin,
1Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi.
2no more in the desires of men, but in the will of God, to live the rest of the time in the flesh;
2Tangu sasa, basi, maisha yaliowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, si na tamaa za kibinadamu.
3for sufficient to us [is] the past time of life the will of the nations to have wrought, having walked in lasciviousnesses, desires, excesses of wines, revelings, drinking-bouts, and unlawful idolatries,
3Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu.
4in which they think it strange — your not running with them to the same excess of dissoluteness, speaking evil,
4Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni.
5who shall give an account to Him who is ready to judge living and dead,
5Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu wazima na wafu!
6for for this also to dead men was good news proclaimed, that they may be judged, indeed, according to men in the flesh, and may live according to God in the spirit.
6Kwa sababu hiyo, hao waliokufa ambao walikuwa wamehukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama anavyohukumiwa kila mmoja, walihubiriwa Habari Njema kusudi katika maisha yao ya kiroho waishi kama aishivyo Mungu.
7And of all things the end hath come nigh; be sober-minded, then, and watch unto the prayers,
7Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na nidhamu, ili mweze kusali.
8and, before all things, to one another having the earnest love, because the love shall cover a multitude of sins;
8Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.
9hospitable to one another, without murmuring;
9Muwe na ukarimu ninyi kwa ninyi bila kunung'unika.
10each, according as he received a gift, to one another ministering it, as good stewards of the manifold grace of God;
10Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile uwakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu.
11if any one doth speak — `as oracles of God;` if any one doth minister — `as of the ability which God doth supply;` that in all things God may be glorified through Jesus Christ, to whom is the glory and the power — to the ages of the ages. Amen.
11Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina.
12Beloved, think it not strange at the fiery suffering among you that is coming to try you, as if a strange thing were happening to you,
12Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
13but, according as ye have fellowship with the sufferings of the Christ, rejoice ye, that also in the revelation of his glory ye may rejoice — exulting;
13Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili mweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
14if ye be reproached in the name of Christ — happy [are ye], because the Spirit of glory and of God upon you doth rest; in regard, indeed, to them, he is evil-spoken of, and in regard to you, he is glorified;
14Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yetu.
15for let none of you suffer as a murderer, or thief, or evil-doer, or as an inspector into other men`s matters;
15Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni muuaji, mwizi, mhalifu au mwovu.
16and if as a Christian, let him not be ashamed; and let him glorify God in this respect;
16Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.
17because it is the time of the beginning of the judgment from the house of God, and if first from us, what the end of those disobedient to the good news of God?
17Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?
18And if the righteous man is scarcely saved, the ungodly and sinner — where shall he appear?
18Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?"
19so that also those suffering according to the will of god, as to a stedfast Creator, let them commit their own souls in good doing.
19Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.