1And I, Paul, myself, do call upon you — through the meekness and gentleness of the Christ — who in presence, indeed [am] humble among you, and being absent, have courage toward you,
1Mimi Paulo mwenyewe ambaye naonekana kuwa mpole nikiwa pamoja nanyi, lakini mkali wakati nikiwa mbali nanyi, nawasihini kwa huruma na wema wake Kristo.
2and I beseech [you], that, being present, I may not have courage, with the confidence with which I reckon to be bold against certain reckoning us as walking according to the flesh;
2Nawaombeni msinisababishe kuwa mkali wakati nitakapokuja, maana nina hakika naweza kuwa mkali kwa wote wale wanaotudhania kwamba tunaishi kidunia.
3for walking in the flesh, not according to the flesh do we war,
3Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia.
4for the weapons of our warfare [are] not fleshly, but powerful to God for bringing down of strongholds,
4Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu za Mungu zenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo,
5reasonings bringing down, and every high thing lifted up against the knowledge of God, and bringing into captivity every thought to the obedience of the Christ,
5na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu ya Mungu; tunaziteka fikira zote na kuzifanya zimtii Kristo.
6and being in readiness to avenge every disobedience, whenever your obedience may be fulfilled.
6Mkisha kuwa wakamilifu katika kutii, sisi tuko tayari kuadhibu kila namna ya kutotii.
7The things in presence do ye see? if any one hath trusted in himself to be Christ`s, this let him reckon again from himself, that according as he is Christ`s, so also we [are] Christ`s;
7Ninyi hutazama mambo kwa nje tu. Je, yupo mtu yeyote anayedhani kwamba yeye ni wa Kristo? Sawa! Basi, afikirie vilevile kwamba sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo wa Kristo.
8for even if also anything more abundantly I shall boast concerning our authority, that the Lord gave us for building up, and not for casting you down, I shall not be ashamed;
8Hata kama nimezidi katika kujivuna kwangu juu ya ule uwezo aliotupa--uwezo wa kuwajenga na sio wa kubomoa--hata hivyo sijutii hata kidogo.
9that I may not seem as if I would terrify you through the letters,
9Sipendi mfikiri kwamba nataka kuwatisha ninyi kwa barua zangu.
10`because the letters indeed — saith one — [are] weighty and strong, and the bodily presence weak, and the speech despicable.`
10Mtu anaweza kusema: "Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito, lakini yeye mwenyewe anapokuwa pamoja nasi ni mtu dhaifu, na hata anapoongea maneno yake ni kama si kitu."
11This one — let him reckon thus: that such as we are in word, through letters, being absent, such also, being present, [we are] in deed.
11Mtu asemaye hivyo heri akumbuke kwamba hakuna tofauti ya yale tunayoandika katika barua wakati tuko mbali, na yale tutakayofanya wakati tutakapokuwa nanyi.
12For we do not make bold to rank or to compare ourselves with certain of those commending themselves, but they, among themselves measuring themselves, and comparing themselves with themselves, are not wise,
12Kwa vyovyote hatungethubutu kujiweka au kujilinganisha na wale watu wanaojisifia wenyewe. Watu wenye kujifanya wao kuwa kipimo cha kujipimia, na watu wanaojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, ni wapumbavu.
13and we in regard to the unmeasured things will not boast ourselves, but after the measure of the line that the God of measure did appoint to us — to reach even unto you;
13Lakini sisi hatutajivuna kupita kiasi; kujivuna huko kutabaki katika kile kipimo cha kazi aliyotukabidhi Mungu, kazi ambayo tunaifanya pia kwenu.
14for not as not reaching to you do we stretch ourselves overmuch, for even unto you did we come in the good news of the Christ,
14Na kwa vile ninyi mu katika mipaka hiyo, hatukuipita tulipokuja kwenu, tukiwaleteeni Habari Njema juu ya Kristo.
15not boasting of the things not measured, in other men`s labours, and having hope — your faith increasing — in you to be enlarged, according to our line — into abundance,
15Basi, hatujivunii kazi waliyofanya wengine zaidi ya kipimo tulichopewa; ila tunatumaini kwamba imani yenu itazidi miongoni mwenu kufuatana na kipimo alichotuwekea Mungu.
16in the [places] beyond you to proclaim good news, not in another`s line in regard to the things made ready, to boast;
16Hapo tutaweza kuihubiri Habari Njema katika nchi nyingine, mbali nanyi; na haitakuwa shauri la kujivunia kazi waliyofanya watu wengine mahali pengine.
17and he who is boasting — in the Lord let him boast;
17Lakini kama yasemavyo Maandiko: "Mwenye kuona fahari na aone fahari juu ya alichofanya Bwana."
18for not he who is commending himself is approved, but he whom the Lord doth commend.
18Anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, bali yule anayesifiwa na Bwana.