1The Elder to Gaius the beloved, whom I love in truth!
1Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2beloved, concerning all things I desire thee to prosper, and to be in health, even as thy soul doth prosper,
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3for I rejoiced exceedingly, brethren coming and testifying of the truth in thee, even as thou in truth dost walk;
3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4greater than these things I have no joy, that I may hear of my children in truth walking.
4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5Beloved, faithfully dost thou do whatever thou mayest work to the brethren and to the strangers,
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6who did testify of thy love before an assembly, whom thou wilt do well, having sent forward worthily of God,
6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7because for [His] name they went forth, nothing receiving from the nations;
7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8we, then, ought to receive such, that fellow-workers we may become to the truth.
8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9I did write to the assembly, but he who is loving the first place among them — Diotrephes — doth not receive us;
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10because of this, if I may come, I will cause him to remember his works that he doth, with evil words prating against us; and not content with these, neither doth he himself receive the brethren, and those intending he doth forbid, and out of the assembly he doth cast.
10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11Beloved, be not thou following that which is evil, but that which is good; he who is doing good, of God he is, and he who is doing evil hath not seen God;
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12to Demetrius testimony hath been given by all, and by the truth itself, and we also — we do testify, and ye have known that our testimony is true.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13Many things I had to write, but I do not wish through ink and pen to write to thee,
13Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14and I hope straightway to see thee, and mouth to mouth we shall speak. Peace to thee! salute thee do the friends; be saluting the friends by name.
14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. (G1-15) Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.