Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Acts

28

1And having been saved, then they knew that the island is called Melita,
1Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2and the foreigners were shewing us no ordinary kindness, for having kindled a fire, they received us all, because of the pressing rain, and because of the cold;
2Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3but Paul having gathered together a quantity of sticks, and having laid [them] upon the fire, a viper — out of the heat having come — did fasten on his hand.
3Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4And when the foreigners saw the beast hanging from his hand, they said unto one another, `Certainly this man is a murderer, whom, having been saved out of the sea, the justice did not suffer to live;`
4Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, "Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!"
5he then, indeed, having shaken off the beast into the fire, suffered no evil,
5Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6and they were expecting him to be about to be inflamed, or to fall down suddenly dead, and they, expecting [it] a long time, and seeing nothing uncommon happening to him, changing [their] minds, said he was a god.
6Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7And in the neighbourhood of that place were lands of the principal man of the island, by name Publius, who, having received us, three days did courteously lodge [us];
7Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8and it came to pass, the father of Publius with feverish heats and dysentery pressed, was laid, unto whom Paul having entered, and having prayed, having laid [his] hands on him, healed him;
8Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9this, therefore, being done, the others also in the island having infirmities were coming and were healed;
9Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10who also with many honours did honour us, and we setting sail — they were lading [us] with the things that were necessary.
10Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11And after three months, we set sail in a ship (that had wintered in the isle) of Alexandria, with the sign Dioscuri,
11Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo "Miungu Pacha". Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12and having landed at Syracuse, we remained three days,
12Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13thence having gone round, we came to Rhegium, and after one day, a south wind having sprung up, the second [day] we came to Puteoli;
13Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14where, having found brethren, we were called upon to remain with them seven days, and thus to Rome we came;
14Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15and thence, the brethren having heard the things concerning us, came forth to meet us, unto Appii Forum, and Three Taverns — whom Paul having seen, having given thanks to God, took courage.
15Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16And when we came to Rome, the centurion delivered up the prisoners to the captain of the barrack, but Paul was suffered to remain by himself, with the soldier guarding him.
16Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17And it came to pass after three days, Paul called together those who are the principal men of the Jews, and they having come together, he said unto them: `Men, brethren, I — having done nothing contrary to the people, or to the customs of the fathers — a prisoner from Jerusalem, was delivered up to the hands of the Romans;
17Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, "Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18who, having examined me, were wishing to release [me], because of their being no cause of death in me,
18Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19and the Jews having spoken against [it], I was constrained to appeal unto Caesar — not as having anything to accuse my nation of;
19Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20for this cause, therefore, I called for you to see and to speak with [you], for because of the hope of Israel with this chain I am bound.`
20Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli."
21And they said unto him, `We did neither receive letters concerning thee from Judea, nor did any one who came of the brethren declare or speak any evil concerning thee,
21Wao wakamwambia, "Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22and we think it good from thee to hear what thou dost think, for, indeed, concerning this sect it is known to us that everywhere it is spoken against;`
22Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali."
23and having appointed him a day, they came, more of them unto him, to the lodging, to whom he was expounding, testifying fully the reign of God, persuading them also of the things concerning Jesus, both from the law of Moses, and the prophets, from morning till evening,
23Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24and, some, indeed, were believing the things spoken, and some were not believing.
24Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25And not being agreed with one another, they were going away, Paul having spoken one word — `Well did the Holy Spirit speak through Isaiah the prophet unto our fathers,
25Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, "Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26saying, Go on unto this people and say, With hearing ye shall hear, and ye shall not understand, and seeing ye shall see, and ye shall not perceive,
26akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27for made gross was the heart of this people, and with the ears they heard heavily, and their eyes they did close, lest they may see with the eyes, and with the heart may understand, and be turned back, and I may heal them.
27Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya."
28`Be it known, therefore, to you, that to the nations was sent the salvation of God, these also will hear it;`
28Halafu Paulo akamaliza na kusema, "Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!"
29and he having said these things, the Jews went away, having much disputation among themselves;
29Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30and Paul remained an entire two years in his own hired [house], and was receiving all those coming in unto him,
30Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31preaching the reign of God, and teaching the things concerning the Lord Jesus Christ with all boldness — unforbidden.
31Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.