Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Acts

4

1And as they are speaking unto the people, there came to them the priests, and the magistrate of the temple, and the Sadducees —
1Petro na Yohane walipokuwa bado wanawahutubia watu, makuhani na mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na Masadukayo walifika.
2being grieved because of their teaching the people, and preaching in Jesus the rising again out of the dead —
2Walikasirika sana, maana hao mitume walikuwa wanawahubiria watu kwamba Yesu alifufuka, jambo ambalo linaonyesha wazi kwamba wafu watafufuka.
3and they laid hands upon them, and did put them in custody unto the morrow, for it was evening already;
3Basi, waliwatia nguvuni na kwa kuwa usiku ulikuwa umekaribia, wakawaweka chini ya ulinzi mpaka kesho yake.
4and many of those hearing the word did believe, and the number of the men became, as it were, five thousand.
4Lakini wengi kati ya wale waliosikia ujumbe wao waliamini, na idadi ya waumini ikawa imefika karibu elfu tano.
5And it came to pass upon the morrow, there were gathered together of them the rulers, and elders, and scribes, to Jerusalem,
5Kesho yake, viongozi wa Wayahudi, wazee na walimu wa Sheria, walikusanyika pamoja huko Yerusalemu.
6and Annas the chief priest, and Caiaphas, and John, and Alexander, and as many as were of the kindred of the chief priest,
6Walikutana pamoja na Anasi, Kayafa, Yohane, Aleksanda na wengine waliokuwa wa ukoo wa Kuhani Mkuu.
7and having set them in the midst, they were inquiring, `In what power, or in what name did ye do this?`
7Waliwasimamisha mitume mbele yao, wakawauliza, "Ninyi mmefanya jambo hili kwa nguvu gani na kwa jina la nani?"
8Then Peter, having been filled with the Holy Spirit, said unto them: `Rulers of the people, and elders of Israel,
8Hapo, Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akawaambia, "Viongozi na wazee wa watu!
9if we to-day are examined concerning the good deed to the ailing man, by whom he hath been saved,
9Ikiwa mnatuuliza leo juu ya kile kitendo chema alichofanyiwa yule mtu aliyekuwa kiwete na jinsi alivyopata kuwa mzima,
10be it known to all of you, and to all the people of Israel, that in the name of Jesus Christ of Nazareth, whom ye did crucify, whom God did raise out of the dead, in him hath this one stood by before you whole.
10basi, ninyi na watu wote wa Israeli mnapaswa kujua kwamba mtu huyu anasimama mbele yenu leo, mzima kabisa, kwa nguvu ya jina lake Yesu wa Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, lakini Mungu akamfufua kutoka wafu.
11`This is the stone that was set at nought by you — the builders, that became head of a corner;
11Huyu ndiye ambaye Maandiko Matakatifu yanasema: Jiwe mlilokataa ninyi waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
12and there is not salvation in any other, for there is no other name under the heaven that hath been given among men, in which it behoveth us to be saved.`
12Wokovu haupatikani kwa mtu mwingine yeyote, kwa maana duniani pote, binadamu hawakupewa jina la mtu mwingine ambaye sisi tunaweza kuokolewa naye."
13And beholding the openness of Peter and John, and having perceived that they are men unlettered and plebeian, they were wondering — they were taking knowledge also of them that with Jesus they had been —
13Hao wazee wa baraza, wakiwa wanajua kwamba Petro na Yohane walikuwa watu wasio na kisomo wala elimu yoyote, walishangaa juu ya jinsi walivyosema kwa uhodari. Wakatambua kwamba walikuwa wamejiunga na Yesu.
14and seeing the man standing with them who hath been healed, they had nothing to say against [it],
14Lakini walipomwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuweza kusema kitu.
15and having commanded them to go away out of the sanhedrim, they took counsel with one another,
15Hivyo, waliwaamuru watoke nje ya baraza, nao wakabaki ndani wakizungumza kwa faragha.
16saying, `What shall we do to these men? because that, indeed, a notable sign hath been done through them, to all those dwelling in Jerusalem [is] manifest, and we are not able to deny [it];
16Wakaulizana, "Tufanye nini na watu hawa? Kila mtu anayeishi Yerusalemu anajua kwamba mwujiza huu wa ajabu umefanyika, nasi hatuwezi kukana jambo hilo.
17but that it may spread no further toward the people, let us strictly threaten them no more to speak in this name to any man.`
17Lakini ili tupate kuzuia jambo hili lisienee zaidi kati ya watu, tuwaonye wasiongee na mtu yeyote kwa jina la Yesu."
18And having called them, they charged them not to speak at all, nor to teach, in the name of Jesus,
18Kwa hiyo wakawaita tena ndani, wakawaonya wasiongee tena hadharani, wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19and Peter and John answering unto them said, `Whether it is righteous before God to hearken to you rather than to God, judge ye;
19Lakini Petro na Yohane wakawajibu, "Amueni ninyi wenyewe kama ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii yeye.
20for we cannot but speak what we did see and hear.`
20Kwa maana hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yale tuliyoyaona na kuyasikia."
21And they having further threatened [them], let them go, finding nothing how they may punish them, because of the people, because all were glorifying God for that which hath been done,
21Basi, hao wazee wa Baraza wakawaonya kwa ukali zaidi, halafu wakawaacha huru. Hawakuweza kuwapa adhabu kwa sababu watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa sababu ya tukio hilo.
22for above forty years of age was the man upon whom had been done this sign of the healing.
22Huyo mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa miaka zaidi ya arobaini.
23And being let go, they went unto their own friends, and declared whatever the chief priests and the elders said unto them,
23Mara tu walipoachwa huru, Petro na Yohane walirudi kwa wenzao, wakawaeleza yale waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee.
24and they having heard, with one accord did lift up the voice unto God, and said, `Lord, thou [art] God, who didst make the heaven, and the earth, and the sea, and all that [are] in them,
24Waliposikia habari hiyo waliungana pamoja katika kumwomba Mungu wakisema, "Bwana, wewe ni Muumba wa mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo!
25who, through the mouth of David thy servant, did say, Why did nations rage, and peoples meditate vain things?
25Ndiwe uliyemfanya mtumishi wako, babu yetu Daudi, aseme kwa nguvu ya Roho Mtakatifu: Kwa nini mataifa yameghadhibika? Mbona watu wamefanya mipango ya bure?
26the kings of the earth stood up, and the rulers were gathered together against the Lord and against His Christ;
26Wafalme wa dunia walijiweka tayari, na watawala walikutana pamoja, ili kumwasi Bwana na Kristo wake.
27for gathered together of a truth against Thy holy child Jesus, whom Thou didst anoint, were both Herod and Pontius Pilate, with nations and peoples of Israel,
27"Maana, kwa hakika, ndivyo Herode, Pontio Pilato, watu wa Israeli na watu wa mataifa walivyokutanika papa hapa mjini, kumpinga Yesu Mtumishi wako Mtakatifu ambaye umemtia mafuta.
28to do whatever Thy hand and Thy counsel did determine before to come to pass.
28Naam, walikutana ili wafanye yale ambayo ulikusudia na kupanga tangu mwanzo kwa uwezo wako na mapenzi yako.
29`And now, Lord, look upon their threatenings, and grant to Thy servants with all freedom to speak Thy word,
29Lakini sasa, ee Bwana, angalia vitisho vyao. Utuwezeshe sisi watumishi wako kuhubiri neno lako kwa uhodari.
30in the stretching forth of Thy hand, for healing, and signs, and wonders, to come to pass through the name of Thy holy child Jesus.`
30Nyosha mkono wako uponye watu. Fanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu Mtumishi wako Mtakatifu."
31And they having prayed, the place was shaken in which they were gathered together, and they were all filled with the Holy Spirit, and were speaking the word of God with freedom,
31Walipomaliza kusali, pale mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, nao wote wakajazwa Roho Mtakatifu. Wote wakaanza kuhubiri neno la Mungu bila uoga.
32and of the multitude of those who did believe the heart and the soul was one, and not one was saying that anything of the things he had was his own, but all things were to them in common.
32Jumuiya yote ya waumini ilikuwa moyo mmoja na roho moja. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na kitu chochote akakiweka kuwa mali yake binafsi, ila waligawana vyote walivyokuwa navyo.
33And with great power were the apostles giving the testimony to the rising again of the Lord Jesus, great grace also was on them all,
33Mitume walishuhudia kwa nguvu nyingi kufufuka kwa Bwana Yesu, naye Mungu akawapa baraka nyingi.
34for there was not any one among them who did lack, for as many as were possessors of fields, or houses, selling [them], were bringing the prices of the thing sold,
34Hakuna mtu yeyote aliyetindikiwa kitu, maana waliokuwa na mashamba au nyumba walikuwa wanaviuza
35and were laying them at the feet of the apostles, and distribution was being made to each according as any one had need.
35na kuwakabidhi mitume fedha hizo, zikagawiwa kila mmoja kadiri ya mahitaji yake.
36And Joses, who was surnamed by the apostles Barnabas — which is, having been interpreted, Son of Comfort — a Levite, of Cyprus by birth,
36Kulikuwa na Mlawi mmoja, mzaliwa wa Kupro, jina lake Yosefu, ambaye mitume walimwita jina Barnaba (maana yake, "Mtu mwenye kutia moyo").
37a field being his, having sold [it], brought the money and laid [it] at the feet of the apostles.
37Yeye pia alikuwa na shamba lake, akaliuza; akazichukua zile fedha, akawakabidhi mitume.