Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Acts

7

1And the chief priest said, `Are then these things so?`
1Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, "Je, mambo haya ni kweli?"
2and he said, `Men, brethren, and fathers, hearken: The God of the glory did appear to our father Abraham, being in Mesopotamia, before his dwelling in Haran,
2Naye Stefano akasema, "Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
3and He said to him, Go forth out of thy land, and out of thy kindred, and come to a land that I shall shew thee.
3Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
4`Then having come forth out of the land of the Chaldeans, he dwelt in Haran, and from thence, after the death of his father, He did remove him to this land wherein ye now dwell,
4Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
5and He gave him no inheritance in it, not even a footstep, and did promise to give it to him for a possession, and to his seed after him — he having no child.
5Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
6`And God spake thus, That his seed shall be sojourning in a strange land, and they shall cause it to serve, and shall do it evil four hundred years,
6Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
7and the nation whom they shall serve I will judge, said God; and after these things they shall come forth and shall do Me service in this place.
7Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
8`And He gave to him a covenant of circumcision, and so he begat Isaac, and did circumcise him on the eighth day, and Isaac [begat] Jacob, and Jacob — the twelve patriarchs;
8Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
9and the patriarchs, having been moved with jealousy, sold Joseph to Egypt, and God was with him,
9"Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
10and did deliver him out of all his tribulations, and gave him favour and wisdom before Pharaoh king of Egypt, and he did set him — governor over Egypt and all his house.
10akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
11`And there came a dearth upon all the land of Egypt and Canaan, and great tribulation, and our fathers were not finding sustenance,
11Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
12and Jacob having heard that there was corn in Egypt, sent forth our fathers a first time;
12Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
13and at the second time was Joseph made known to his brethren, and Joseph`s kindred became manifest to Pharaoh,
13Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
14and Joseph having sent, did call for his father Jacob, and all his kindred — with seventy and five souls —
14Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
15and Jacob went down to Egypt, and died, himself and our fathers,
15Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
16and they were carried over into Sychem, and were laid in the tomb that Abraham bought for a price in money from the sons of Emmor, of Sychem.
16Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17`And according as the time of the promise was drawing nigh, which God did swear to Abraham, the people increased and multiplied in Egypt,
17"Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
18till another king rose, who had not known Joseph;
18Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
19this one, having dealt subtilely with our kindred, did evil to our fathers, causing to expose their babes, that they might not live;
19Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
20in which time Moses was born, and he was fair to God, and he was brought up three months in the house of his father;
20Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
21and he having been exposed, the daughter of Pharaoh took him up, and did rear him to herself for a son;
21na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
22and Moses was taught in all wisdom of the Egyptians, and he was powerful in words and in works.
22Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
23`And when forty years were fulfilled to him, it came upon his heart to look after his brethren, the sons of Israel;
23"Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
24and having seen a certain one suffering injustice, he did defend, and did justice to the oppressed, having smitten the Egyptian;
24Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
25and he was supposing his brethren to understand that God through his hand doth give salvation; and they did not understand.
25(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
26`On the succeeding day, also, he shewed himself to them as they are striving, and urged them to peace, saying, Men, brethren are ye, wherefore do ye injustice to one another?
26Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
27and he who is doing injustice to the neighbour, did thrust him away, saying, Who set thee a ruler and a judge over us?
27Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
28to kill me dost thou wish, as thou didst kill yesterday the Egyptian?
28Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
29`And Moses fled at this word, and became a sojourner in the land of Midian, where he begat two sons,
29Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
30and forty years having been fulfilled, there appeared to him in the wilderness of mount Sinai a messenger of the Lord, in a flame of fire of a bush,
30"Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
31and Moses having seen did wonder at the sight; and he drawing near to behold, there came a voice of the Lord unto him,
31Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
32I [am] the God of thy fathers; the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob. `And Moses having become terrified, durst not behold,
32Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
33and the Lord said to him, Loose the sandal of thy feet, for the place in which thou hast stood is holy ground;
33Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
34seeing I have seen the affliction of My people that [is] in Egypt, and their groaning I did hear, and came down to deliver them; and now come, I will send thee to Egypt.
34Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
35`This Moses, whom they did refuse, saying, Who did set thee a ruler and a judge? this one God a ruler and a redeemer did send, in the hand of a messenger who appeared to him in the bush;
35"Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
36this one did bring them forth, having done wonders and signs in the land of Egypt, and in the Red Sea, and in the wilderness forty years;
36Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
37this is the Moses who did say to the sons of Israel: A prophet to you shall the Lord your God raise up out of your brethren, like to me, him shall ye hear.
37Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
38`This is he who was in the assembly in the wilderness, with the messenger who is speaking to him in the mount Sinai, and with our fathers who did receive the living oracles to give to us;
38Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
39to whom our fathers did not wish to become obedient, but did thrust away, and turned back in their hearts to Egypt,
39"Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
40saying to Aaron, Make to us gods who shall go on before us, for this Moses, who brought us forth out of the land of Egypt, we have not known what hath happened to him.
40Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
41`And they made a calf in those days, and brought a sacrifice to the idol, and were rejoicing in the works of their hands,
41Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
42and God did turn, and did give them up to do service to the host of the heaven, according as it hath been written in the scroll of the prophets: Slain beasts and sacrifices did ye offer to Me forty years in the wilderness, O house of Israel?
42Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
43and ye took up the tabernacle of Moloch, and the star of your god Remphan — the figures that ye made to bow before them, and I will remove your dwelling beyond Babylon.
43Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
44`The tabernacle of the testimony was among our fathers in the wilderness, according as He did direct, who is speaking to Moses, to make it according to the figure that he had seen;
44Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
45which also our fathers having in succession received, did bring in with Joshua, into the possession of the nations whom God did drive out from the presence of our fathers, till the days of David,
45Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
46who found favour before God, and requested to find a tabernacle for the God of Jacob;
46Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
47and Solomon built Him an house.
47Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
48`But the Most High in sanctuaries made with hands doth not dwell, according as the prophet saith:
48"Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
49The heaven [is] My throne, and the earth My footstool; what house will ye build to Me? saith the Lord, or what [is] the place of My rest?
49Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
50hath not My hand made all these things?
50Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
51`Ye stiff-necked and uncircumcised in heart and in ears! ye do always the Holy Spirit resist; as your fathers — also ye;
51"Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
52which of the prophets did not your fathers persecute? and they killed those who declared before about the coming of the Righteous One, of whom now ye betrayers and murderers have become,
52Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
53who received the law by arrangement of messengers, and did not keep [it].`
53Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii."
54And hearing these things, they were cut to the hearts, and did gnash the teeth at him;
54Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
55and being full of the Holy Spirit, having looked stedfastly to the heaven, he saw the glory of God, and Jesus standing on the right hand of God,
55Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
56and he said, `Lo, I see the heavens having been opened, and the Son of Man standing on the right hand of God.`
56Akasema, "Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu."
57And they, having cried out with a loud voice, stopped their ears, and did rush with one accord upon him,
57Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
58and having cast him forth outside of the city, they were stoning [him] — and the witnesses did put down their garments at the feet of a young man called Saul —
58wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
59and they were stoning Stephen, calling and saying, `Lord Jesus, receive my spirit;`
59Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: "Bwana Yesu, ipokee roho yangu!"
60and having bowed the knees, he cried with a loud voice, `Lord, mayest thou not lay to them this sin;` and this having said, he fell asleep.
60Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: "Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii." Baada ya kusema hivyo, akafa.