Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Ephesians

6

1The children! obey your parents in the Lord, for this is righteous;
1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2honour thy father and mother,
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3which is the first command with a promise, `That it may be well with thee, and thou mayest live a long time upon the land.`
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
4And the fathers! provoke not your children, but nourish them in the instruction and admonition of the Lord.
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5The servants! obey the masters according to the flesh with fear and trembling, in the simplicity of your heart, as to the Christ;
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6not with eye-service as men-pleasers, but as servants of the Christ, doing the will of God out of soul,
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7with good-will serving, as to the Lord, and not to men,
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8having known that whatever good thing each one may do, this he shall receive from the Lord, whether servant or freeman.
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9And the masters! the same things do ye unto them, letting threatening alone, having known that also your Master is in the heavens, and acceptance of persons is not with him.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10As to the rest, my brethren, be strong in the Lord, and in the power of his might;
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11put on the whole armour of God, for your being able to stand against the wiles of the devil,
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12because we have not the wrestling with blood and flesh, but with the principalities, with the authorities, with the world-rulers of the darkness of this age, with the spiritual things of the evil in the heavenly places;
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
13because of this take ye up the whole armour of God, that ye may be able to resist in the day of the evil, and all things having done — to stand.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14Stand, therefore, having your loins girt about in truth, and having put on the breastplate of the righteousness,
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15and having the feet shod in the preparation of the good-news of the peace;
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16above all, having taken up the shield of the faith, in which ye shall be able all the fiery darts of the evil one to quench,
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17and the helmet of the salvation receive, and the sword of the Spirit, which is the saying of God,
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18through all prayer and supplication praying at all times in the Spirit, and in regard to this same, watching in all perseverance and supplication for all the saints —
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19and in behalf of me, that to me may be given a word in the opening of my mouth, in freedom, to make known the secret of the good news,
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20for which I am an ambassador in a chain, that in it I may speak freely — as it behoveth me to speak.
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21And that ye may know — ye also — the things concerning me — what I do, all things make known to you shall Tychicus, the beloved brother and faithful ministrant in the Lord,
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22whom I did send unto you for this very thing, that ye might know the things concerning us, and that he might comfort your hearts.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23Peace to the brethren, and love, with faith, from God the Father, and the Lord Jesus Christ!
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24The grace with all those loving our Lord Jesus Christ — undecayingly! Amen.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.