1For the law having a shadow of the coming good things — not the very image of the matters, every year, by the same sacrifices that they offer continually, is never able to make perfect those coming near,
1Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2since, would they not have ceased to be offered, because of those serving having no more conscience of sins, having once been purified?
2Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3but in those [sacrifices] is a remembrance of sins every year,
3Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4for it is impossible for blood of bulls and goats to take away sins.
4Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5Wherefore, coming into the world, he saith, `Sacrifice and offering Thou didst not will, and a body Thou didst prepare for me,
5Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: "Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6in burnt-offerings, and concerning sin-offerings, Thou didst not delight,
6Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7then I said, Lo, I come, (in a volume of the book it hath been written concerning me,) to do, O God, Thy will;`
7Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria."
8saying above — `Sacrifice, and offering, and burnt-offerings, and concerning sin-offering Thou didst not will, nor delight in,` — which according to the law are offered —
8Kwanza alisema: "Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi." Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9then he said, `Lo, I come to do, O God, Thy will;` he doth take away the first that the second he may establish;
9Kisha akasema: "Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako." Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10in the which will we are having been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once,
10Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11and every priest, indeed, hath stood daily serving, and the same sacrifices many times offering, that are never able to take away sins.
11Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12And He, for sin one sacrifice having offered — to the end, did sit down on the right hand of God, —
12Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13as to the rest, expecting till He may place his enemies [as] his footstool,
13Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14for by one offering he hath perfected to the end those sanctified;
14Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15and testify to us also doth the Holy Spirit, for after that He hath said before,
15Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16`This [is] the covenant that I will make with them after those days, saith the Lord, giving My laws on their hearts, and upon their minds I will write them,`
16"Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao."
17and `their sins and their lawlessness I will remember no more;`
17Kisha akaongeza kusema: "Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu."
18and where forgiveness of these [is], there is no more offering for sin.
18Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19Having, therefore, brethren, boldness for the entrance into the holy places, in the blood of Jesus,
19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20which way he did initiate for us — new and living, through the vail, that is, his flesh —
20Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21and a high priest over the house of God,
21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22may we draw near with a true heart, in full assurance of faith, having the hearts sprinkled from an evil conscience, and having the body bathed with pure water;
22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23may we hold fast the unwavering profession of the hope, (for faithful [is] He who did promise),
23Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24and may we consider one another to provoke to love and to good works,
24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25not forsaking the assembling of ourselves together, as a custom of certain [is], but exhorting, and so much the more as ye see the day coming nigh.
25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26For we — willfully sinning after the receiving the full knowledge of the truth — no more for sins doth there remain a sacrifice,
26Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27but a certain fearful looking for of judgment, and fiery zeal, about to devour the opposers;
27Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28any one who did set at nought a law of Moses, apart from mercies, by two or three witnesses, doth die,
28Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29of how much sorer punishment shall he be counted worthy who the Son of God did trample on, and the blood of the covenant did count a common thing, in which he was sanctified, and to the Spirit of the grace did despite?
29Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30for we have known Him who is saying, `Vengeance [is] Mine, I will recompense, saith the Lord;` and again, `The Lord shall judge His people;` —
30Maana tunamfahamu yule aliyesema, "Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza," na ambaye alisema pia, "Bwana atawahukumu watu wake."
31fearful [is] the falling into the hands of a living God.
31Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32And call to your remembrance the former days, in which, having been enlightened, ye did endure much conflict of sufferings,
32Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33partly both with reproaches and tribulations being made spectacles, and partly having become partners of those so living,
33Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34for also with my bonds ye sympathised, and the robbery of your goods with joy ye did receive, knowing that ye have in yourselves a better substance in the heavens, and an enduring one.
34Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35Ye may not cast away, then, your boldness, which hath great recompense of reward,
35Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36for of patience ye have need, that the will of God having done, ye may receive the promise,
36Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37for yet a very very little, He who is coming will come, and will not tarry;
37Maana kama yasemavyo Maandiko: "Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38and `the righteous by faith shall live,` and `if he may draw back, My soul hath no pleasure in him,`
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye."
39and we are not of those drawing back to destruction, but of those believing to a preserving of soul.
39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.