Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Hebrews

13

1Let brotherly love remain;
1Endeleeni kupendana kidugu.
2of the hospitality be not forgetful, for through this unawares certain did entertain messengers;
2Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3be mindful of those in bonds, as having been bound with them, of those maltreated, as also yourselves being in the body;
3Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4honourable [is] the marriage in all, and the bed undefiled, and whoremongers and adulterers God shall judge.
4Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5Without covetousness the behaviour, being content with the things present, for He hath said, `No, I will not leave, no, nor forsake thee,`
5Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
6so that we do boldly say, `The Lord [is] to me a helper, and I will not fear what man shall do to me.`
6Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
7Be mindful of those leading you, who did speak to you the word of God, whose faith — considering the issue of the behaviour — be imitating,
7wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8Jesus Christ yesterday and to-day the same, and to the ages;
8Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
9with teachings manifold and strange be not carried about, for [it is] good that by grace the heart be confirmed, not with meats, in which they who were occupied were not profited;
9Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10we have an altar, of which to eat they have no authority who the tabernacle are serving,
10Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11for of those beasts whose blood is brought for sin into the holy places through the chief priest — of these the bodies are burned without the camp.
11Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12Wherefore, also Jesus — that he might sanctify through [his] own blood the people — without the gate did suffer;
12Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13now, then, may we go forth unto him without the camp, his reproach bearing;
13Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14for we have not here an abiding city, but the coming one we seek;
14Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15through him, then, we may offer up a sacrifice of praise always to God, that is, the fruit of lips, giving thanks to His name;
15Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16and of doing good, and of fellowship, be not forgetful, for with such sacrifices God is well-pleased.
16Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17Be obedient to those leading you, and be subject, for these do watch for your souls, as about to give account, that with joy they may do this, and not sighing, for this [is] unprofitable to you.
17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18Pray for us, for we trust that we have a good conscience, in all things willing to behave well,
18Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19and more abundantly do I call upon [you] to do this, that more quickly I may be restored to you.
19Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20And the God of the peace, who did bring up out of the dead the great shepherd of the sheep — in the blood of an age-during covenant — our Lord Jesus,
20Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele.
21make you perfect in every good work to do His will, doing in you that which is well-pleasing before Him, through Jesus Christ, to whom [is] the glory — to the ages of the ages! Amen.
21Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
22And I entreat you, brethren, suffer the word of the exhortation, for also through few words I have written to you.
22Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23Know ye that the brother Timotheus is released, with whom, if he may come more shortly, I will see you.
23Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24Salute all those leading you, and all the saints; salute you doth those from Italy:
24Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25the grace [is] with you all! Amen.
25Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.