Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

James

2

1My brethren, hold not, in respect of persons, the faith of the glory of our Lord Jesus Christ,
1Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2for if there may come into your synagogue a man with gold ring, in gay raiment, and there may come in also a poor man in vile raiment,
2Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3and ye may look upon him bearing the gay raiment, and may say to him, `Thou — sit thou here well,` and to the poor man may say, `Thou — stand thou there, or, Sit thou here under my footstool,` —
3Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: "Keti hapa mahali pazuri," na kumwambia yule maskini: "Wewe, simama huko," au "Keti hapa sakafuni miguuni pangu,"
4ye did not judge fully in yourselves, and did become ill-reasoning judges.
4je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5Hearken, my brethren beloved, did not God choose the poor of this world, rich in faith, and heirs of the reign that He promised to those loving Him?
5Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6and ye did dishonour the poor one; do not the rich oppress you and themselves draw you to judgment-seats;
6Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7do they not themselves speak evil of the good name that was called upon you?
7Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8If, indeed, royal law ye complete, according to the Writing, `Thou shalt love thy neighbour as thyself,` — ye do well;
8Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: "Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9and if ye accept persons, sin ye do work, being convicted by the law as transgressors;
9Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10for whoever the whole law shall keep, and shall stumble in one [point], he hath become guilty of all;
10Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11for He who is saying, `Thou mayest not commit adultery,` said also, `Thou mayest do no murder;` and if thou shalt not commit adultery, and shalt commit murder, thou hast become a transgressor of law;
11Maana yuleyule aliyesema: "Usizini," alisema pia "Usiue". Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12so speak ye and so do, as about by a law of liberty to be judged,
12Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13for the judgment without kindness [is] to him not having done kindness, and exult doth kindness over judgment.
13Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14What [is] the profit, my brethren, if faith, any one may speak of having, and works he may not have? is that faith able to save him?
14Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15and if a brother or sister may be naked, and may be destitute of the daily food,
15Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16and any one of you may say to them, `Depart ye in peace, be warmed, and be filled,` and may not give to them the things needful for the body, what [is] the profit?
16Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: "Nendeni salama mkaote moto na kushiba," bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17so also the faith, if it may not have works, is dead by itself.
17Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18But say may some one, Thou hast faith, and I have works, shew me thy faith out of thy works, and I will shew thee out of my works my faith:
18Lakini mtu anaweza kusema: "Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!" Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19thou — thou dost believe that God is one; thou dost well, and the demons believe, and they shudder!
19Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20And dost thou wish to know, O vain man, that the faith apart from the works is dead?
20Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21Abraham our father — was not he declared righteous out of works, having brought up Isaac his son upon the altar?
21Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22dost thou see that the faith was working with his works, and out of the works the faith was perfected?
22Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23and fulfilled was the Writing that is saying, `And Abraham did believe God, and it was reckoned to him — to righteousness;` and, `Friend of God` he was called.
23Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: "Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu."
24Ye see, then, that out of works is man declared righteous, and not out of faith only;
24Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25and in like manner also Rahab the harlot — was she not out of works declared righteous, having received the messengers, and by another way having sent forth?
25Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26for as the body apart from the spirit is dead, so also the faith apart from the works is dead.
26Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.