Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

James

5

1Go, now, ye rich! weep, howling over your miseries that are coming upon [you];
1Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
2your riches have rotted, and your garments have become moth-eaten;
2Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
3your gold and silver have rotted, and the rust of them for a testimony shall be to you, and shall eat your flesh as fire. Ye made treasure in the last days!
3Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
4lo, the reward of the workmen, of those who in-gathered your fields, which hath been fraudulently kept back by you — doth cry out, and the exclamations of those who did reap into the ears of the Lord of Sabaoth have entered;
4Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
5ye did live in luxury upon the earth, and were wanton; ye did nourish your hearts, as in a day of slaughter;
5Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
6ye did condemn — ye did murder the righteous one, he doth not resist you.
6Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
7Be patient, then, brethren, till the presence of the Lord; lo, the husbandman doth expect the precious fruit of the earth, being patient for it, till he may receive rain — early and latter;
7Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
8be patient, ye also; establish your hearts, because the presence of the Lord hath drawn nigh;
8Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
9murmur not against one another, brethren, that ye may not be condemned; lo, the Judge before the door hath stood.
9Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
10An example take ye of the suffering of evil, my brethren, and of the patience, the prophets who did speak in the name of the Lord;
10Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
11lo, we call happy those who are enduring; the endurance of Job ye heard of, and the end of the Lord ye have seen, that very compassionate is the Lord, and pitying.
11Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
12And before all things, my brethren, do not swear, neither by the heaven, neither by the earth, neither by any other oath, and let your Yes be Yes, and the No, No; that under judgment ye may not fall.
12Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni "Ndiyo" kama maana yenu ni ndiyo, na "La" kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
13Doth any one suffer evil among you? let him pray; is any of good cheer? let him sing psalms;
13Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
14is any infirm among you? let him call for the elders of the assembly, and let them pray over him, having anointed him with oil, in the name of the Lord,
14Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15and the prayer of the faith shall save the distressed one, and the Lord shall raise him up, and if sins he may have committed, they shall be forgiven to him.
15Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
16Be confessing to one another the trespasses, and be praying for one another, that ye may be healed; very strong is a working supplication of a righteous man;
16Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
17Elijah was a man like affected as we, and with prayer he did pray — not to rain, and it did not rain upon the land three years and six months;
17Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18and again he did pray, and the heaven did give rain, and the land did bring forth her fruit.
18Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
19Brethren, if any among you may go astray from the truth, and any one may turn him back,
19Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
20let him know that he who did turn back a sinner from the straying of his way shall save a soul from death, and shall cover a multitude of sins.
20fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.