Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

John

4

1When therefore the Lord knew that the Pharisees heard that Jesus more disciples doth make and baptize than John,
1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2(though indeed Jesus himself was not baptizing, but his disciples,)
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3he left Judea and went away again to Galilee,
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4and it was behoving him to go through Samaria.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5He cometh, therefore, to a city of Samaria, called Sychar, near to the place that Jacob gave to Joseph his son;
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6and there was there a well of Jacob. Jesus therefore having been weary from the journeying, was sitting thus on the well; it was as it were the sixth hour;
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7there cometh a woman out of Samaria to draw water. Jesus saith to her, `Give me to drink;`
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
8for his disciples were gone away to the city, that they may buy victuals;
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9the Samaritan woman therefore saith to him, `How dost thou, being a Jew, ask drink from me, being a Samaritan woman?` for Jews have no dealing with Samaritans.
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10Jesus answered and said to her, `If thou hadst known the gift of God, and who it is who is saying to thee, Give me to drink, thou wouldest have asked him, and he would have given thee living water.`
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
11The woman saith to him, `Sir, thou hast not even a vessel to draw with, and the well is deep; whence, then, hast thou the living water?
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12Art thou greater than our father Jacob, who did give us the well, and himself out of it did drink, and his sons, and his cattle?`
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
13Jesus answered and said to her, `Every one who is drinking of this water shall thirst again;
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14but whoever may drink of the water that I will give him, may not thirst — to the age; and the water that I will give him shall become in him a well of water, springing up to life age-during.`
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
15The woman saith unto him, `Sir, give me this water, that I may not thirst, nor come hither to draw.`
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
16Jesus saith to her, `Go, call thy husband, and come hither;`
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
17the woman answered and said, `I have not a husband.` Jesus saith to her, `Well didst thou say — A husband I have not;
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
18for five husbands thou hast had, and, now, he whom thou hast is not thy husband; this hast thou said truly.`
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
19The woman saith to him, `Sir, I perceive that thou art a prophet;
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20our fathers in this mountain did worship, and ye — ye say that in Jerusalem is the place where it behoveth to worship.`
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
21Jesus saith to her, `Woman, believe me, that there doth come an hour, when neither in this mountain, nor in Jerusalem, shall ye worship the Father;
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22ye worship what ye have not known; we worship what we have known, because the salvation is of the Jews;
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23but, there cometh an hour, and it now is, when the true worshippers will worship the Father in spirit and truth, for the Father also doth seek such to worship him;
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24God [is] a Spirit, and those worshipping Him, in spirit and truth it doth behove to worship.`
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
25The woman saith to him, `I have known that Messiah doth come, who is called Christ, when that one may come, he will tell us all things;`
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
26Jesus saith to her, `I am [he], who am speaking to thee.`
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
27And upon this came his disciples, and were wondering that with a woman he was speaking, no one, however, said, `What seekest thou?` or `Why speakest thou with her?`
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
28The woman then left her water-jug, and went away to the city, and saith to the men,
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29`Come, see a man, who told me all things — as many as I did; is this the Christ?`
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
30They went forth therefore out of the city, and were coming unto him.
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31And in the meanwhile his disciples were asking him, saying, `Rabbi, eat;`
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
32and he said to them, `I have food to eat that ye have not known.`
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
33The disciples then said one to another, `Did any one bring him anything to eat?`
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
34Jesus saith to them, `My food is, that I may do the will of Him who sent me, and may finish His work;
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35do not say that it is yet four months, and the harvest cometh; lo, I say to you, Lift up your eyes, and see the fields, that they are white unto harvest already.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36`And he who is reaping doth receive a reward, and doth gather fruit to life age-during, that both he who is sowing and he who is reaping may rejoice together;
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
37for in this the saying is the true one, that one is the sower and another the reaper.
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38I sent you to reap that on which ye have not laboured; others laboured, and ye into their labour have entered.
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
39And from that city many believed in him, of the Samaritans, because of the word of the woman testifying, — `He told me all things — as many as I did.`
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
40When, then, the Samaritans came unto him, they were asking him to remain with them, and he remained there two days;
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41and many more did believe because of his word,
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42and said to the woman — `No more because of thy speaking do we believe; for we ourselves have heard and known that this is truly the Saviour of the world — the Christ.`
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
43And after the two days he went forth thence, and went away to Galilee,
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44for Jesus himself testified that a prophet in his own country shall not have honour;
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
45when then, he came to Galilee, the Galileans received him, having seen all things that he did in Jerusalem in the feast — for they also went to the feast.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46Jesus came, therefore, again to Cana of Galilee, where he made the water wine, and there was a certain courtier, whose son was ailing in Capernaum,
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47he, having heard that Jesus is come out of Judea to Galilee, went away unto him, and was asking him that he may come down and may heal his son, for he was about to die.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48Jesus then said unto him, `If signs and wonders ye may not see, ye will not believe.`
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
49The courtier saith unto him, `Sir, come down before my child die;`
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
50Jesus saith to him, `Be going on; thy son doth live.` And the man believed the word that Jesus said to him, and was going on,
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51and he now going down, his servants met him, and told, saying — `Thy child doth live;`
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52he inquired then of them the hour in which he became better, and they said to him — `Yesterday at the seventh hour the fever left him;`
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
53then the father knew that [it was] in that hour in which Jesus said to him — `Thy son doth live,` and he himself believed, and his whole house;
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54this again a second sign did Jesus, having come out of Judea to Galilee.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.