Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Luke

12

1At which time the myriads of the multitude having been gathered together, so as to tread upon one another, he began to say unto his disciples, first, `Take heed to yourselves of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy;
1Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, "Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2and there is nothing covered, that shall not be revealed; and hid, that shall not be known;
2Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3because whatever in the darkness ye said, in the light shall be heard: and what to the ear ye spake in the inner-chambers, shall be proclaimed upon the house-tops.
3Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4`And I say to you, my friends, be not afraid of those killing the body, and after these things are not having anything over to do;
4"Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5but I will show to you, whom ye may fear; Fear him who, after the killing, is having authority to cast to the gehenna; yes, I say to you, Fear ye Him.
5Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo.
6`Are not five sparrows sold for two assars? and one of them is not forgotten before God,
6Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7but even the hairs of your head have been all numbered; therefore fear ye not, than many sparrows ye are of more value.
7Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8`And I say to you, Every one — whoever may confess with me before men, the Son of Man also shall confess with him before the messengers of God,
8"Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9and he who hath denied me before men, shall be denied before the messengers of God,
9Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10and every one whoever shall say a word to the Son of Man, it shall be forgiven to him, but to him who to the Holy Spirit did speak evil, it shall not be forgiven.
10"Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11`And when they bring you before the synagogues, and the rulers, and the authorities, be not anxious how or what ye may reply, or what ye may say,
11"Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12for the Holy Spirit shall teach you in that hour what it behoveth [you] to say.`
12Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema."
13And a certain one said to him, out of the multitude, `Teacher, say to my brother to divide with me the inheritance.`
13Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, "Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba."
14And he said to him, `Man, who set me a judge or a divider over you?`
14Yesu akamjibu, "Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?"
15And he said unto them, `Observe, and beware of the covetousness, because not in the abundance of one`s goods is his life.`
15Basi, akawaambia wote, "Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo."
16And he spake a simile unto them, saying, `Of a certain rich man the field brought forth well;
16Kisha akawaambia mfano: "Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17and he was reasoning within himself, saying, What shall I do, because I have not where I shall gather together my fruits?
17Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18and he said, This I will do, I will take down my storehouses, and greater ones I will build, and I will gather together there all my products and my good things,
18Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19and I will say to my soul, Soul, thou hast many good things laid up for many years, be resting, eat, drink, be merry.
19Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20`And God said to him, Unthinking one! this night thy soul they shall require from thee, and what things thou didst prepare — to whom shall they be?
20Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?"
21so [is] he who is treasuring up to himself, and is not rich toward God.`
21Yesu akamaliza kwa kusema "Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu."
22And he said unto his disciples, `Because of this, to you I say, Be not anxious for your life, what ye may eat; nor for the body, what ye may put on;
22Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23the life is more than the nourishment, and the body than the clothing.
23Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24`Consider the ravens, that they sow not, nor reap, to which there is no barn nor storehouse, and God doth nourish them; how much better are ye than the fowls?
24Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25and who of you, being anxious, is able to add to his age one cubit?
25Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26If, then, ye are not able for the least — why for the rest are ye anxious?
26Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27`Consider the lilies, how do they grow? they labour not, nor do they spin, and I say to you, not even Solomon in all his glory was arrayed as one of these;
27Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28and if the herbage in the field, that to-day is, and to-morrow into an oven is cast, God doth so clothe, how much more you — ye of little faith?
28Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29`And ye — seek not what ye may eat, or what ye may drink, and be not in suspense,
29"Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30for all these things do the nations of the world seek after, and your Father hath known that ye have need of these things;
30Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31but, seek ye the reign of God, and all these things shall be added to you.
31Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32`Fear not, little flock, because your Father did delight to give you the reign;
32"Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33sell your goods, and give alms, make to yourselves bags that become not old, a treasure unfailing in the heavens, where thief doth not come near, nor moth destroy;
33Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34for where your treasure is, there also your heart will be.
34Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35`Let your loins be girded, and the lamps burning,
35"Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36and ye like to men waiting for their lord, when he shall return out of the wedding feasts, that he having come and knocked, immediately they may open to him.
36muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37`Happy those servants, whom the lord, having come, shall find watching; verily I say to you, that he will gird himself, and will cause them to recline (at meat), and having come near, will minister to them;
37Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38and if he may come in the second watch, and in the third watch he may come, and may find [it] so, happy are those servants.
38Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39`And this know, that if the master of the house had known what hour the thief doth come, he would have watched, and would not have suffered his house to be broken through;
39Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40and ye, then, become ye ready, because at the hour ye think not, the Son of Man doth come.`
40Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
41And Peter said to him, `Sir, unto us this simile dost thou speak, or also unto all?`
41Petro akamwambia, "Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?"
42And the Lord said, `Who, then, is the faithful and prudent steward whom the lord shall set over his household, to give in season the wheat measure?
42Bwana akajibu, "Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43Happy that servant, whom his lord, having come, shall find doing so;
43Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44truly I say to you, that over all his goods he will set him.
44Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45`And if that servant may say in his heart, My lord doth delay to come, and may begin to beat the men-servants and the maid-servants, to eat also, and to drink, and to be drunken;
45Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46the lord of that servant will come in a day in which he doth not look for [him], and in an hour that he doth not know, and will cut him off, and his portion with the unfaithful he will appoint.
46bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47`And that servant, who having known his lord`s will, and not having prepared, nor having gone according to his will, shall be beaten with many stripes,
47Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48and he who, not having known, and having done things worthy of stripes, shall be beaten with few; and to every one to whom much was given, much shall be required from him; and to whom they did commit much, more abundantly they will ask of him.
48Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49`Fire I came to cast to the earth, and what will I if already it was kindled?
49"Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50but I have a baptism to be baptized with, and how am I pressed till it may be completed!
50Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51`Think ye that peace I came to give in the earth? no, I say to you, but rather division;
51Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52for there shall be henceforth five in one house divided — three against two, and two against three;
52Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53a father shall be divided against a son, and a son against a father, a mother against a daughter, and a daughter against a mother, a mother-in-law against her daughter-in-law, and a daughter-in-law against her mother-in-law.`
53Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake."
54And he said also to the multitudes, `When ye may see the cloud rising from the west, immediately ye say, A shower doth come, and it is so;
54Yesu akayaambia tena makundi ya watu, "Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55and when — a south wind blowing, ye say, that there will be heat, and it is;
55Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56hypocrites! the face of the earth and of the heaven ye have known to make proof of, but this time — how do ye not make proof of [it]?
56Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57`And why, also, of yourselves, judge ye not what is righteous?
57"Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58for, as thou art going away with thy opponent to the ruler, in the way give diligence to be released from him, lest he may drag thee unto the judge, and the judge may deliver thee to the officer, and the officer may cast thee into prison;
58Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59I say to thee, thou mayest not come forth thence till even the last mite thou mayest give back.`
59Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho."