Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Luke

4

1And Jesus, full of the Holy Spirit, turned back from the Jordan, and was brought in the Spirit to the wilderness,
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2forty days being tempted by the Devil, and he did not eat anything in those days, and they having been ended, he afterward hungered,
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3and the Devil said to him, `If Son thou art of God, speak to this stone that it may become bread.`
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4And Jesus answered him, saying, `It hath been written, that, not on bread only shall man live, but on every saying of God.`
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5And the Devil having brought him up to an high mountain, shewed to him all the kingdoms of the world in a moment of time,
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6and the Devil said to him, `To thee I will give all this authority, and their glory, because to me it hath been delivered, and to whomsoever I will, I do give it;
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7thou, then, if thou mayest bow before me — all shall be thine.`
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8And Jesus answering him said, `Get thee behind me, Adversary, for it hath been written, Thou shalt bow before the Lord thy God, and Him only thou shalt serve.`
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9And he brought him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, `If the Son thou art of God, cast thyself down hence,
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10for it hath been written — To His messengers He will give charge concerning thee, to guard over thee,
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11and — On hands they shall bear thee up, lest at any time thou mayest dash against a stone thy foot.`
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12And Jesus answering said to him — `It hath been said, Thou shalt not tempt the Lord thy God.`
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13And having ended all temptation, the Devil departed from him till a convenient season.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14And Jesus turned back in the power of the Spirit to Galilee, and a fame went forth through all the region round about concerning him,
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15and he was teaching in their synagogues, being glorified by all.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16And he came to Nazareth, where he hath been brought up, and he went in, according to his custom, on the sabbath-day, to the synagogue, and stood up to read;
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17and there was given over to him a roll of Isaiah the prophet, and having unfolded the roll, he found the place where it hath been written:
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18`The Spirit of the Lord [is] upon me, Because He did anoint me; To proclaim good news to the poor, Sent me to heal the broken of heart, To proclaim to captives deliverance, And to blind receiving of sight, To send away the bruised with deliverance,
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19To proclaim the acceptable year of the Lord.`
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20And having folded the roll, having given [it] back to the officer, he sat down, and the eyes of all in the synagogue were gazing on him.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21And he began to say unto them — `To-day hath this writing been fulfilled in your ears;`
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22and all were bearing testimony to him, and were wondering at the gracious words that are coming forth out of his mouth, and they said, `Is not this the son of Joseph?`
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23And he said unto them, `Certainly ye will say to me this simile, Physician, heal thyself; as great things as we heard done in Capernaum, do also here in thy country;`
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24and he said, `Verily I say to you — No prophet is accepted in his own country;
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25and of a truth I say to you, Many widows were in the days of Elijah, in Israel, when the heaven was shut for three years and six months, when great famine came on all the land,
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26and unto none of them was Elijah sent, but — to Sarepta of Sidon, unto a woman, a widow;
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27and many lepers were in the time of Elisha the prophet, in Israel, and none of them was cleansed, but — Naaman the Syrian.`
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28And all in the synagogue were filled with wrath, hearing these things,
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29and having risen, they put him forth without the city, and brought him unto the brow of the hill on which their city had been built — to cast him down headlong,
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30and he, having gone through the midst of them, went away.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31And he came down to Capernaum, a city of Galilee, and was teaching them on the sabbaths,
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32and they were astonished at his teaching, because his word was with authority.
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33And in the synagogue was a man, having a spirit of an unclean demon, and he cried out with a great voice,
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34saying, `Away, what — to us and to thee, Jesus, O Nazarene? thou didst come to destroy us; I have known thee who thou art — the Holy One of God.`
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35And Jesus did rebuke him, saying, `Be silenced, and come forth out of him;` and the demon having cast him into the midst, came forth from him, having hurt him nought;
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36and amazement came upon all, and they were speaking together, with one another, saying, `What [is] this word, that with authority and power he doth command the unclean spirits, and they come forth?`
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37and there was going forth a fame concerning him to every place of the region round about.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38And having risen out of the synagogue, he entered into the house of Simon, and the mother-in-law of Simon was pressed with a great fever, and they did ask him about her,
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39and having stood over her, he rebuked the fever, and it left her, and presently, having risen, she was ministering to them.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40And at the setting of the sun, all, as many as had any ailing with manifold sicknesses, brought them unto him, and he on each one of them [his] hands having put, did heal them.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41And demons also were coming forth from many, crying out and saying — `Thou art the Christ, the Son of God;` and rebuking, he did not suffer them to speak, because they knew him to be the Christ.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42And day having come, having gone forth, he went on to a desert place, and the multitudes were seeking him, and they came unto him, and were staying him — not to go on from them,
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43and he said unto them — `Also to the other cities it behoveth me to proclaim good news of the reign of God, because for this I have been sent;`
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44and he was preaching in the synagogues of Galilee.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.