1And the passover and the unleavened food were after two days, and the chief priests and the scribes were seeking how, by guile, having taken hold of him, they might kill him;
1Ilikuwa siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
2and they said, `Not in the feast, lest there shall be a tumult of the people.`
2Lakini walisema, "Tusimtie nguvuni wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia."
3And he, being in Bethany, in the house of Simon the leper, at his reclining (at meat), there came a woman having an alabaster box of ointment, of spikenard, very precious, and having broken the alabaster box, did pour on his head;
3Yesu alikuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, Mkoma. Alipokuwa mezani kula chakula, mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya nardo safi ya thamani kubwa alikuja, akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu marashi hayo kichwani.
4and there were certain much displeased within themselves, and saying, `For what hath this waste of the ointment been made?
4Baadhi ya watu waliokuwa hapo walikasirika wakajisemea, "Kwa nini kupoteza ovyo marashi haya?
5for this could have been sold for more than three hundred denaries, and given to the poor;` and they were murmuring at her.
5Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha denari mia tatu, wakapewa maskini!" Wakamkemea huyo mama.
6And Jesus said, `Let her alone; why are ye giving her trouble? a good work she wrought on me;
6Lakini Yesu akawaambia, "Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.
7for the poor always ye have with you, and whenever ye may will ye are able to do them good, but me ye have not always;
7Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
8what she could she did, she anticipated to anoint my body for the embalming.
8Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa maziko.
9Verily I say to you, wherever this good news may be proclaimed in the whole world, what also this woman did shall be spoken of — for a memorial of her.`
9Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa ajili ya kumkumbuka."
10And Judas the Iscariot, one of the twelve, went away unto the chief priests that he might deliver him up to them,
10Kisha Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, alienda kwa makuhani wakuu ili kumsaliti Yesu.
11and having heard, they were glad, and promised to give him money, and he was seeking how, conveniently, he might deliver him up.
11Makuhani wakuu waliposikia habari hiyo, walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Basi, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.
12And the first day of the unleavened food, when they were killing the passover, his disciples say to him, `Where wilt thou, [that,] having gone, we may prepare, that thou mayest eat the passover?`
12Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wakati ambapo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza, "Wataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?"
13And he sendeth forth two of his disciples, and saith to them, `Go ye away to the city, and there shall meet you a man bearing a pitcher of water, follow him;
13Basi Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake akiwaambia, "Nendeni mjini, nanyi mtakutana na mtu anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni
14and wherever he may go in, say ye to the master of the house — The Teacher saith, Where is the guest-chamber, where the passover, with my disciples, I may eat?
14mpaka katika nyumba atakayoingia, mkamwambie mwenye nyumba, Mwalimu anasema: wapi chumba changu ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
15and he will shew you a large upper room, furnished, prepared — there make ready for us.`
15Naye atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichotayarishwa na kupambwa. Tuandalieni humo."
16And his disciples went forth, and came to the city, and found as he said to them, and they made ready the passover.
16Wanafunzi wakaondoka, wakaenda mjini, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Wakaandaa karamu ya Pasaka.
17And evening having come, he cometh with the twelve,
17Ilipokuwa jioni, Yesu alifika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
18and as they are reclining, and eating, Jesus said, `Verily I say to you — one of you, who is eating with me — shall deliver me up.`
18Walipokuwa mezani wakila, Yesu alisema, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti."
19And they began to be sorrowful, and to say to him, one by one, `Is it I?` and another, `Is it I?`
19Hapo wanafunzi wake wakaanza kuhuzunika, wakamwuliza mmojammoja, "Je, ni mimi?"
20And he answering said to them, `One of the twelve who is dipping with me in the dish;
20Yesu akawaambia, "Ni mmoja wenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli.
21the Son of Man doth indeed go, as it hath been written concerning him, but wo to that man through whom the Son of Man is delivered up; good were it to him if that man had not been born.`
21Kweli Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake; lakini, ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa!"
22And as they are eating, Jesus having taken bread, having blessed, brake, and gave to them, and said, `Take, eat; this is my body.`
22Walipokuwa wanakula, Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni; huu ni mwili wangu."
23And having taken the cup, having given thanks, he gave to them, and they drank of it — all;
23Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa; nao wote wakanywa katika kikombe hicho.
24and he said to them, `This is my blood of the new covenant, which for many is being poured out;
24Akawaambia, "Hii ni damu yangu inayothibitisha agano la Mungu, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi.
25verily I say to you, that no more may I drink of the produce of the vine till that day when I may drink it new in the reign of God.`
25Kweli nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa upya katika Ufalme wa Mungu."
26And having sung an hymn, they went forth to the mount of the Olives,
26Kisha wakaimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
27and Jesus saith to them — `All ye shall be stumbled at me this night, because it hath been written, I will smite the shepherd, and the sheep shall be scattered abroad,
27Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami; maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji nao kondoo watatawanyika.
28but after my having risen I will go before you to Galilee.`
28Lakini nikisha fufuka, nitawatangulieni kule Galilaya."
29And Peter said to him, `And if all shall be stumbled, yet not I;`
29Petro akamwambia "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakukana kamwe!"
30And Jesus said to him, `Verily I say to thee, that to-day, this night, before a cock shall crow twice, thrice thou shalt deny me.`
30Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu."
31And he spake the more vehemently, `If it may be necessary for me to die with thee — I will in nowise deny thee;` and in like manner also said they all.
31Lakini Petro akasisitiza, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakuacha kamwe." Wanafunzi wote pia wakasema vivyo hivyo.
32And they come to a spot, the name of which [is] Gethsemane, and he saith to his disciples, `Sit ye here till I may pray;`
32Basi, wakafika katika bustani iitwayo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa wakati mimi nasali."
33and he taketh Peter, and James, and John with him, and began to be amazed, and to be very heavy,
33Kisha akawachukua Petro, Yakobo na Yohane; akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
34and he saith to them, `Exceeding sorrowful is my soul — to death; remain here, and watch.`
34Akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe."
35And having gone forward a little, he fell upon the earth, and was praying, that, if it be possible the hour may pass from him,
35Akaenda mbele kidogo, akajitupa chini kifudifudi, akasali kwamba, kama ingewezekana, asiipitie saa hiyo ya mateso.
36and he said, `Abba, Father; all things are possible to Thee; make this cup pass from me; but, not what I will, but what Thou.`
36Akasema, "Baba yangu, kwako mambo yote yanawezekana. Uniondolee kikombe hiki; lakini isiwe kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe."
37And he cometh, and findeth them sleeping, and saith to Peter, `Simon, thou dost sleep! thou wast not able to watch one hour!
37Kisha akarudi kwa wanafunzi wale watatu, akawakuta wamelala. Basi, akamwuliza Petro, "Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?"
38Watch ye and pray, that ye may not enter into temptation; the spirit indeed is forward, but the flesh weak.`
38Kisha akawaambia, "Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu."
39And again having gone away, he prayed, the same word saying;
39Akaenda kusali tena akirudia maneno yaleyale.
40and having returned, he found them again sleeping, for their eyes were heavy, and they had not known what they might answer him.
40Kisha akarudi tena, akawakuta wamelala. Macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Hawakujua la kumjibu.
41And he cometh the third time, and saith to them, `Sleep on henceforth, and rest — it is over; the hour did come; lo, the Son of Man is delivered up to the hands of the sinful;
41Alipowajia mara ya tatu aliwaambia, "Mnalala bado na kupumzika? Sasa imetosha! Saa imefika! Mwana wa Mtu anakabidhiwa kwa watu waovu.
42rise, we may go, lo, he who is delivering me up hath come nigh.`
42Amkeni, twendeni zetu. Tazameni, yule atakayenisaliti amekaribia."
43And immediately — while he is yet speaking — cometh near Judas, one of the twelve, and with him a great multitude, with swords and sticks, from the chief priests, and the scribes, and the elders;
43Yesu alipokuwa bado anasema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee.
44and he who is delivering him up had given a token to them, saying, `Whomsoever I shall kiss, he it is, lay hold on him, and lead him away safely,`
44Msaliti Yuda alikuwa amewapa ishara: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni, mkampeleke chini ya ulinzi."
45and having come, immediately, having gone near him, he saith, `Rabbi, Rabbi,` and kissed him.
45Yuda alipofika tu, alimwendea Yesu moja kwa moja, akasema, "Mwalimu!" Kisha akambusu.
46And they laid on him their hands, and kept hold on him;
46Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
47and a certain one of those standing by, having drawn the sword, struck the servant of the chief priest, and took off his ear.
47Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
48And Jesus answering said to them, `As against a robber ye came out, with swords and sticks, to take me!
48Yesu akawaambia, "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
49daily I was with you in the temple teaching, and ye did not lay hold on me — but that the Writings may be fulfilled.`
49Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie."
50And having left him they all fled;
50Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
51and a certain young man was following him, having put a linen cloth about [his] naked body, and the young men lay hold on him,
51Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.
52and he, having left the linen cloth, did flee from them naked.
52Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.
53And they led away Jesus unto the chief priest, and come together to him do all the chief priests, and the elders, and the scribes;
53Basi, wakampeleka Yesu kwa Kuhani Mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na walimu wa Sheria walikuwa wamekutanika.
54and Peter afar off did follow him, to the inside of the hall of the chief priest, and he was sitting with the officers, and warming himself near the fire.
54Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ya wa Kuhani Mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.
55And the chief priests and all the sanhedrim were seeking against Jesus testimony — to put him to death, and they were not finding,
55Makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu wapate kumwua, lakini hawakupata.
56for many were bearing false testimony against him, and their testimonies were not alike.
56Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
57And certain having risen up, were bearing false testimony against him, saying —
57Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
58`We heard him saying — I will throw down this sanctuary made with hands, and by three days, another made without hands I will build;`
58"Tulimsikia mtu huyu akisema, Nitaliharibu Hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono."
59and neither so was their testimony alike.
59Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.
60And the chief priest, having risen up in the midst, questioned Jesus, saying, `Thou dost not answer anything! what do these testify against thee?`
60Basi, Kuhani Mkuu akasimama katikati yao, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
61and he was keeping silent, and did not answer anything. Again the chief priest was questioning him, and saith to him, `Art thou the Christ — the Son of the Blessed?`
61Lakini yeye akakaa kimya; hakusema hata neno moja. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, "Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Mtukufu?"
62and Jesus said, `I am; and ye shall see the Son of Man sitting on the right hand of the power, and coming with the clouds, of the heaven.`
62Yesu akajibu, "Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenyezi, akija katika mawingu ya mbinguni."
63And the chief priest, having rent his garments, saith, `What need have we yet of witnesses?
63Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, "Tuna haja gani tena ya mashahidi?
64Ye heard the evil speaking, what appeareth to you?` and they all condemned him to be worthy of death,
64Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?" Wote wakaamua kwamba anastahili kuuawa.
65and certain began to spit on him, and to cover his face, and to buffet him, and to say to him, `Prophesy;` and the officers were striking him with their palms.
65Basi, baadhi yao wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, wakampiga na kumwambia, "Bashiri ni nani aliyekupiga!" Hata watumishi wakamchukua, wakampiga makofi.
66And Peter being in the hall beneath, there doth come one of the maids of the chief priest,
66Petro alipokuwa bado chini ukumbini, mmoja wa wajakazi wa kuhani Mkuu alikuja.
67and having seen Peter warming himself, having looked on him, she said, `And thou wast with Jesus of Nazareth!`
67Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama, akamwambia, "Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti."
68and he denied, saying, `I have not known [him], neither do I understand what thou sayest;` and he went forth without to the porch, and a cock crew.
68Lakini Petro akakana, "Sijui, wala sielewi unayosema!" Kisha Petro akaondoka, akaenda nje uani. Hapo jogoo akawika.
69And the maid having seen him again, began to say to those standing near — `This is of them;`
69Yule mjakazi alipomwona tena Petro, akaanza tena kuwaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, "Mtu huyu ni mmoja wao."
70and he was again denying. And after a little again, those standing near said to Peter, `Truly thou art of them, for thou also art a Galilean, and thy speech is alike;`
70Petro akakana tena. Baadaye kidogo, watu waliokuwa wamesimama hapo wakamwambia Petro, "Hakika wewe ni mmoja wao, maana wewe ni Mgalilaya."
71and he began to anathematize, and to swear — `I have not known this man of whom ye speak;`
71Lakini Petro akaanza kulaani na kuapa akisema, "Mimi simjui mtu huyu mnayesema habari zake."
72and a second time a cock crew, and Peter remembered the saying that Jesus said to him — `Before a cock crow twice, thou mayest deny me thrice;` and having thought thereon — he was weeping.
72Hapo jogoo akawika mara ya pili. Basi, Petro akakumbuka jinsi Yesu alivyokuwa amemwambia: "Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu." Petro akabubujika machozi.