Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Mark

2

1And again he entered into Capernaum, after [some] days, and it was heard that he is in the house,
1Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
2and immediately many were gathered together, so that there was no more room, not even at the door, and he was speaking to them the word.
2Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
3And they come unto him, bringing a paralytic, borne by four,
3wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
4and not being able to come near to him because of the multitude, they uncovered the roof where he was, and, having broken [it] up, they let down the couch on which the paralytic was lying,
4Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
5and Jesus having seen their faith, saith to the paralytic, `Child, thy sins have been forgiven thee.`
5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako."
6And there were certain of the scribes there sitting, and reasoning in their hearts,
6Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
7`Why doth this one thus speak evil words? who is able to forgive sins except one — God?`
7"Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake."
8And immediately Jesus, having known in his spirit that they thus reason in themselves, said to them, `Why these things reason ye in your hearts?
8Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9which is easier, to say to the paralytic, The sins have been forgiven to thee? or to say, Rise, and take up thy couch, and walk?
9Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
10`And, that ye may know that the Son of Man hath authority on the earth to forgive sins — (he saith to the paralytic) —
10Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
11I say to thee, Rise, and take up thy couch, and go away to thy house;`
11"Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!"
12and he rose immediately, and having taken up the couch, he went forth before all, so that all were astonished, and do glorify God, saying — `Never thus did we see.`
12Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, "Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili."
13And he went forth again by the sea, and all the multitude was coming unto him, and he was teaching them,
13Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
14and passing by, he saw Levi of Alpheus sitting at the tax-office, and saith to him, `Be following me,` and he, having risen, did follow him.
14Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, "Nifuate!" Lawi akasimama, akamfuata.
15And it came to pass, in his reclining (at meat) in his house, that many tax-gatherers and sinners were reclining (at meat) with Jesus and his disciples, for there were many, and they followed him.
15Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
16And the scribes and the Pharisees, having seen him eating with the tax-gatherers and sinners, said to his disciples, `Why — that with the tax-gatherers and sinners he doth eat and drink?`
16Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, "Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
17And Jesus, having heard, saith to them, `They who are strong have no need of a physician, but they who are ill; I came not to call righteous men, but sinners to reformation.`
17Yesu alipowasikia, akawaambia, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi."
18And the disciples of John and those of the Pharisees were fasting, and they come and say to him, `Wherefore do the disciples of John and those of the Pharisees fast, and thy disciples do not fast?`
18Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, "Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?"
19And Jesus said to them, `Are the sons of the bride-chamber able, while the bridegroom is with them, to fast? so long time as they have the bridegroom with them they are not able to fast;
19Yesu akajibu, "Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
20but days shall come when the bridegroom may be taken from them, and then they shall fast — in those days.
20Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
21`And no one a patch of undressed cloth doth sew on an old garment, and if not — the new filling it up doth take from the old and the rent doth become worse;
21"Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
22and no one doth put new wine into old skins, and if not — the new wine doth burst the skins, and the wine is poured out, and the skins will be destroyed; but new wine into new skins is to be put.`
22Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!"
23And it came to pass — he is going along on the sabbaths through the corn-fields — and his disciples began to make a way, plucking the ears,
23Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
24and the Pharisees said to him, `Lo, why do they on the sabbaths that which is not lawful?`
24Mafarisayo wakawaambia, "Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?"
25And he said to them, `Did ye never read what David did, when he had need and was hungry, he and those with him?
25Yesu akawajibu, "Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
26how he went into the house of God, (at `Abiathar the chief priest,`) and the loaves of the presentation did eat, which it is not lawful to eat, except to the priests, and he gave also to those who were with him?`
26naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake."
27And he said to them, `The sabbath for man was made, not man for the sabbath,
27Basi, Yesu akawaambia, "Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
28so that the son of man is lord also of the sabbath.`
28Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato."