1And again he began to teach by the sea, and there was gathered unto him a great multitude, so that he, having gone into the boat, sat in the sea, and all the multitude was near the sea, on the land,
1Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
2and he taught them many things in similes, and he said to them in his teaching:
2Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
3`Hearken, lo, the sower went forth to sow;
3"Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4and it came to pass, in the sowing, some fell by the way, and the fowls of the heaven did come and devour it;
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5and other fell upon the rocky ground, where it had not much earth, and immediately it sprang forth, because of not having depth of earth,
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6and the sun having risen, it was scorched, and because of not having root it did wither;
6Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7and other fell toward the thorns, and the thorns did come up, and choke it, and fruit it gave not;
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
8and other fell to the good ground, and was giving fruit, coming up and increasing, and it bare, one thirty-fold, and one sixty, and one an hundred.`
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia."
9And he said to them, `He who is having ears to hear — let him hear.`
9Kisha akawaambia, "Mwenye masikio na asikie!"
10And when he was alone, those about him, with the twelve, did ask him of the simile,
10Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
11and he said to them, `To you it hath been given to know the secret of the reign of God, but to those who are without, in similes are all the things done;
11Naye akawaambia, "Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
12that seeing they may see and not perceive, and hearing they may hear and not understand, lest they may turn, and the sins may be forgiven them.`
12ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe."
13And he saith to them, `Have ye not known this simile? and how shall ye know all the similes?
13Basi, Yesu akawauliza, "Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
14He who is sowing doth sow the word;
14Mpanzi hupanda neno la Mungu.
15and these are they by the way where the word is sown: and whenever they may hear, immediately cometh the Adversary, and he taketh away the word that hath been sown in their hearts.
15Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
16`And these are they, in like manner, who on the rocky ground are sown: who, whenever they may hear the word, immediately with joy do receive it,
16Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
17and have not root in themselves, but are temporary; afterward tribulation or persecution having come because of the word, immediately they are stumbled.
17Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
18`And these are they who toward the thorns are sown: these are they who are hearing the word,
18Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
19and the anxieties of this age, and the deceitfulness of the riches, and the desires concerning the other things, entering in, choke the word, and it becometh unfruitful.
19lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda.
20`And these are they who on the good ground have been sown: who do hear the word, and receive, and do bear fruit, one thirty-fold, and one sixty, and one an hundred.`
20Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja."
21And he said to them, `Doth the lamp come that under the measure it may be put, or under the couch — not that it may be put on the lamp-stand?
21Yesu akaendelea kuwaambia, "Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
22for there is not anything hid that may not be manifested, nor was anything kept hid but that it may come to light.
22Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
23If any hath ears to hear — let him hear.`
23Mwenye masikio na asikie!"
24And he said to them, `Take heed what ye hear; in what measure ye measure, it shall be measured to you; and to you who hear it shall be added;
24Akawaambia pia, "Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
25for whoever may have, there shall be given to him, and whoever hath not, also that which he hath shall be taken from him.`
25Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa."
26And he said, `Thus is the reign of God: as if a man may cast the seed on the earth,
26Yesu akaendelea kusema, "Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
27and may sleep, and may rise night and day, and the seed spring up and grow, he hath not known how;
27Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
28for of itself doth the earth bear fruit, first a blade, afterwards an ear, afterwards full corn in the ear;
28Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
29and whenever the fruit may yield itself, immediately he doth send forth the sickle, because the harvest hath come.`
29Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika."
30And he said, `To what may we liken the reign of God, or in what simile may we compare it?
30Tena, Yesu akasema, "Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
31As a grain of mustard, which, whenever it may be sown on the earth, is less than any of the seeds that are on the earth;
31Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
32and whenever it may be sown, it cometh up, and doth become greater than any of the herbs, and doth make great branches, so that under its shade the fowls of the heaven are able to rest.`
32Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake."
33And with many such similes he was speaking to them the word, as they were able to hear,
33Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
34and without a simile he was not speaking to them, and by themselves, to his disciples he was expounding all.
34Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
35And he saith to them on that day, evening having come, `We may pass over to the other side;`
35Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, "Tuvuke ziwa, twende ng'ambo."
36and having let away the multitude, they take him up as he was in the boat, and other little boats also were with him.
36Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
37And there cometh a great storm of wind, and the waves were beating on the boat, so that it is now being filled,
37Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
38and he himself was upon the stern, upon the pillow sleeping, and they wake him up, and say to him, `Teacher, art thou not caring that we perish?`
38Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, "Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?"
39And having waked up, he rebuked the wind, and said to the sea, `Peace, be stilled;` and the wind did lull, and there was a great calm:
39Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, "Kimya! Tulia!" Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
40and he said to them, `Why are ye so fearful? how have ye not faith?`
40Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?"
41and they feared a great fear, and said one to another, `Who, then, is this, that even the wind and the sea do obey him?`
41Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, "Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?"