1And after six days Jesus taketh Peter, and James, and John his brother, and doth bring them up to a high mount by themselves,
1Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
2and he was transfigured before them, and his face shone as the sun, and his garments did become white as the light,
2Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3and lo, appear to them did Moses and Elijah, talking together with him.
3Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
4And Peter answering said to Jesus, `Sir, it is good to us to be here; if thou wilt, we may make here three booths — for thee one, and for Moses one, and one for Elijah.`
4Hapo Petro akamwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
5While he is yet speaking, lo, a bright cloud overshadowed them, and lo, a voice out of the cloud, saying, `This is My Son, — the Beloved, in whom I did delight; hear him.`
5Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni."
6And the disciples having heard, did fall upon their face, and were exceedingly afraid,
6Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
7and Jesus having come near, touched them, and said, `Rise, be not afraid,`
7Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, "Simameni, msiogope!"
8and having lifted up their eyes, they saw no one, except Jesus only.
8Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
9And as they are coming down from the mount, Jesus charged them, saying, `Say to no one the vision, till the Son of Man out of the dead may rise.`
9Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: "Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu."
10And his disciples questioned him, saying, `Why then do the scribes say that Elijah it behoveth to come first?`
10Kisha wanafunzi wakamwuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?"
11And Jesus answering said to them, `Elijah doth indeed come first, and shall restore all things,
11Yesu akawajibu, "Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
12and I say to you — Elijah did already come, and they did not know him, but did with him whatever they would, so also the Son of Man is about to suffer by them.`
12Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao."
13Then understood the disciples that concerning John the Baptist he spake to them.
13Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
14And when they came unto the multitude, there came to him a man, kneeling down to him,
14Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
15and saying, `Sir, deal kindly with my son, for he is lunatic, and doth suffer miserably, for often he doth fall into the fire, and often into the water,
15akasema, "Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
16and I brought him near to thy disciples, and they were not able to heal him.`
16Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya."
17And Jesus answering said, `O generation, unstedfast and perverse, till when shall I be with you? till when shall I bear you? bring him to me hither;`
17Yesu akajibu, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto."
18and Jesus rebuked him, and the demon went out of him, and the lad was healed from that hour.
18Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
19Then the disciples having come to Jesus by himself, said, `Wherefore were we not able to cast him out?`
19Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?"
20And Jesus said to them, `Through your want of faith; for verily I say to you, if ye may have faith as a grain of mustard, ye shall say to this mount, Remove hence to yonder place, and it shall remove, and nothing shall be impossible to you,
20Yesu akawajibu, "Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu."
21and this kind doth not go forth except in prayer and fasting.`
21"Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga."
22And while they are living in Galilee, Jesus said to them, `The Son of Man is about to be delivered up to the hands of men,
22Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
23and they shall kill him, and the third day he shall rise,` and they were exceeding sorry.
23Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa." Wanafunzi wakahuzunika mno.
24And they having come to Capernaum, those receiving the didrachms came near to Peter, and said, `Your teacher — doth he not pay the didrachms?` He saith, `Yes.`
24Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, "Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?"
25And when he came into the house, Jesus anticipated him, saying, `What thinkest thou, Simon? the kings of the earth — from whom do they receive custom or poll-tax? from their sons or from the strangers?`
25Petro akajibu, "Naam, hulipa." Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, "Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?"
26Peter saith to him, `From the strangers.` Jesus said to him, `Then are the sons free;
26Petro akajibu, "Kutoka kwa wageni." Yesu akamwambia, "Haya basi, wananchi hawahusiki.
27but, that we may not cause them to stumble, having gone to the sea, cast a hook, and the fish that hath come up first take thou up, and having opened its mouth, thou shalt find a stater, that having taken, give to them for me and thee.`
27Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako."