Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Matthew

20

1`For the reign of the heavens is like to a man, a householder, who went forth with the morning to hire workmen for his vineyard,
1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2and having agreed with the workmen for a denary a day, he sent them into his vineyard.
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3`And having gone forth about the third hour, he saw others standing in the market-place idle,
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4and to these he said, Go ye — also ye — to the vineyard, and whatever may be righteous I will give you;
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5and they went away. `Again, having gone forth about the sixth and the ninth hour, he did in like manner.
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6And about the eleventh hour, having gone forth, he found others standing idle, and saith to them, Why here have ye stood all the day idle?
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7they say to him, Because no one did hire us; he saith to them, Go ye — ye also — to the vineyard, and whatever may be righteous ye shall receive.
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8`And evening having come, the lord of the vineyard saith to his steward, Call the workmen, and pay them the reward, having begun from the last — unto the first.
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9And they of about the eleventh hour having come, did receive each a denary.
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10`And the first having come, did suppose that they shall receive more, and they received, they also, each a denary,
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11and having received [it], they were murmuring against the householder, saying,
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12that These, the last, wrought one hour, and thou didst make them equal to us, who were bearing the burden of the day — and the heat.
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13`And he answering said to one of them, Comrade, I do no unrighteousness to thee; for a denary didst not thou agree with me?
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14take that which is thine, and go; and I will to give to this, the last, also as to thee;
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15is it not lawful to me to do what I will in mine own? is thine eye evil because I am good?
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
16So the last shall be first, and the first last, for many are called, and few chosen.`
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
17And Jesus going up to Jerusalem, took the twelve disciples by themselves in the way, and said to them,
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18`Lo, we go up to Jerusalem, and the Son of Man shall be delivered to the chief priests and scribes,
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19and they shall condemn him to death, and shall deliver him to the nations to mock, and to scourge, and to crucify, and the third day he will rise again.`
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
20Then came near to him the mother of the sons of Zebedee, with her sons, bowing and asking something from him,
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21and he said to her, `What wilt thou?` She saith to him, `Say, that they may sit — these my two sons — one on thy right hand, and one on the left, in thy reign.`
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
22And Jesus answering said, `Ye have not known what ye ask for yourselves; are ye able to drink of the cup that I am about to drink? and with the baptism that I am baptized with, to be baptized?` They say to him, `We are able.`
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
23And he saith to them, `Of my cup indeed ye shall drink, and with the baptism that I am baptized with ye shall be baptized; but to sit on my right hand and on my left is not mine to give, but — to those for whom it hath been prepared by my father.`
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
24And the ten having heard, were much displeased with the two brothers,
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25and Jesus having called them near, said, `Ye have known that the rulers of the nations do exercise lordship over them, and those great do exercise authority over them,
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26but not so shall it be among you, but whoever may will among you to become great, let him be your ministrant;
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27and whoever may will among you to be first, let him be your servant;
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28even as the Son of Man did not come to be ministered to, but to minister, and to give his life a ransom for many.`
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
29And they going forth from Jericho, there followed him a great multitude,
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30and lo, two blind men sitting by the way, having heard that Jesus doth pass by, cried, saying, `Deal kindly with us, sir — Son of David.`
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31And the multitude charged them that they might be silent, and they cried out the more, saying, `Deal kindly with us sir — Son of David.`
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
32And having stood, Jesus called them, and said, `What will ye [that] I may do to you?`
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
33they say to him, `Sir, that our eyes may be opened;`
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
34and having been moved with compassion, Jesus touched their eyes, and immediately their eyes received sight, and they followed him.
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.