1`Take heed your kindness not to do before men, to be seen by them, and if not — reward ye have not from your Father who [is] in the heavens;
1"Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
2whenever, therefore, thou mayest do kindness, thou mayest not sound a trumpet before thee as the hypocrites do, in the synagogues, and in the streets, that they may have glory from men; verily I say to you — they have their reward!
2"Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
3`But thou, doing kindness, let not thy left hand know what thy right hand doth,
3Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
4that thy kindness may be in secret, and thy Father who is seeing in secret Himself shall reward thee manifestly.
4Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
5`And when thou mayest pray, thou shalt not be as the hypocrites, because they love in the synagogues, and in the corners of the broad places — standing — to pray, that they may be seen of men; verily I say to you, that they have their reward.
5"Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
6`But thou, when thou mayest pray, go into thy chamber, and having shut thy door, pray to thy Father who [is] in secret, and thy Father who is seeing in secret, shall reward thee manifestly.
6Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
7`And — praying — ye may not use vain repetitions like the nations, for they think that in their much speaking they shall be heard,
7"Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
8be ye not therefore like to them, for your Father doth know those things that ye have need of before your asking him;
8Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
9thus therefore pray ye: `Our Father who [art] in the heavens! hallowed be Thy name.
9Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
10`Thy reign come: Thy will come to pass, as in heaven also on the earth.
10Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
11`Our appointed bread give us to-day.
11Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
12`And forgive us our debts, as also we forgive our debtors.
12Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
13`And mayest Thou not lead us to temptation, but deliver us from the evil, because Thine is the reign, and the power, and the glory — to the ages. Amen.
13Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
14`For, if ye may forgive men their trespasses He also will forgive you — your Father who [is] in the heavens;
14"Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15but if ye may not forgive men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16`And when ye may fast, be ye not as the hypocrites, of sour countenances, for they disfigure their faces, that they may appear to men fasting; verily I say to you, that they have their reward.
16"Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
17`But thou, fasting, anoint thy head, and wash thy face,
17Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
18that thou mayest not appear to men fasting, but to thy Father who [is] in secret, and thy Father, who is seeing in secret, shall reward thee manifestly.
18ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
19`Treasure not up to yourselves treasures on the earth, where moth and rust disfigure, and where thieves break through and steal,
19"Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
20but treasure up to yourselves treasures in heaven, where neither moth nor rust doth disfigure, and where thieves do not break through nor steal,
20Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
21for where your treasure is, there will be also your heart.
21Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
22`The lamp of the body is the eye, if, therefore, thine eye may be perfect, all thy body shall be enlightened,
22"Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
23but if thine eye may be evil, all thy body shall be dark; if, therefore, the light that [is] in thee is darkness — the darkness, how great!
23Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
24`None is able to serve two lords, for either he will hate the one and love the other, or he will hold to the one, and despise the other; ye are not able to serve God and Mammon.
24"Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
25`Because of this I say to you, be not anxious for your life, what ye may eat, and what ye may drink, nor for your body, what ye may put on. Is not the life more than the nourishment, and the body than the clothing?
25"Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
26look to the fowls of the heaven, for they do not sow, nor reap, nor gather into storehouses, and your heavenly Father doth nourish them; are not ye much better than they?
26Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
27`And who of you, being anxious, is able to add to his age one cubit?
27Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
28and about clothing why are ye anxious? consider well the lilies of the field; how do they grow? they do not labour, nor do they spin;
28"Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
29and I say to you, that not even Solomon in all his glory was arrayed as one of these.
29Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
30`And if the herb of the field, that to-day is, and to-morrow is cast to the furnace, God doth so clothe — not much more you, O ye of little faith?
30Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
31therefore ye may not be anxious, saying, What may we eat? or, What may we drink? or, What may we put round?
31"Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
32for all these do the nations seek for, for your heavenly Father doth know that ye have need of all these;
32Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
33but seek ye first the reign of God and His righteousness, and all these shall be added to you.
33Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
34Be not therefore anxious for the morrow, for the morrow shall be anxious for its own things; sufficient for the day [is] the evil of it.
34Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.