1Let every soul to the higher authorities be subject, for there is no authority except from God, and the authorities existing are appointed by God,
1Kila mtu anapaswa kuwatii wenye mamlaka katika serikali; maana mamlaka yote hutoka kwa Mungu; nao wenye mamlaka wamewekwa na Mungu.
2so that he who is setting himself against the authority, against God`s ordinance hath resisted; and those resisting, to themselves shall receive judgment.
2Anayepinga mamlaka ya viongozi anapinga agizo la Mungu; nao wafanyao hivyo wanajiletea hukumu wenyewe,
3For those ruling are not a terror to the good works, but to the evil; and dost thou wish not to be afraid of the authority? that which is good be doing, and thou shalt have praise from it,
3Maana, watawala hawasababishi hofu kwa watu wema, ila kwa watu wabaya. Basi, wataka usimwogope mtu mwenye mamlaka? Fanya mema naye atakusifu;
4for of God it is a ministrant to thee for good; and if that which is evil thou mayest do, be fearing, for not in vain doth it bear the sword; for of God it is a ministrant, an avenger for wrath to him who is doing that which is evil.
4maana yeye ni mtumishi wa Mungu anayefanya kazi kwa faida yako. Lakini ukifanya mabaya, basi, huna budi kumwogopa, maana anao kweli uwezo wa kutoa adhabu. Yeye ni mtumishi wa Mungu na huitekeleza ghadhabu ya Mungu kwao watendao maovu.
5Wherefore it is necessary to be subject, not only because of the wrath, but also because of the conscience,
5Kwa hiyo ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si tu kwa sababu ya kuogopa ghadhabu ya Mungu, bali pia kwa sababu dhamiri inadai hivyo.
6for because of this also pay ye tribute; for servants of God they are, on this very thing attending continually;
6Kwa sababu hiyohiyo ninyi hulipa kodi; maana viongozi hao humtumikia Mungu ikiwa wanatimiza wajibu wao.
7render, therefore, to all [their] dues; to whom tribute, the tribute; to whom custom, the custom; to whom fear, the fear; to whom honour, the honour.
7Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.
8To no one owe anything, except to love one another; for he who is loving the other — law he hath fulfilled,
8Msiwe na deni kwa mtu yeyote, isipokuwa tu deni la kupendana. Ampendaye jirani yake ameitekeleza Sheria.
9for, `Thou shalt not commit adultery, Thou shalt do no murder, Thou shalt not steal, Thou shalt not bear false testimony, Thou shalt not covet;` and if there is any other command, in this word it is summed up, in this: `Thou shalt love thy neighbor as thyself;`
9Maana, amri hizi: "Usizini; Usiue; Usitamani;" na nyingine zote, zimo katika amri hii moja: "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
10the love to the neighbor doth work no ill; the love, therefore, [is] the fulness of law.
10Ampendaye jirani yake hamtendei vibaya. Basi, kwa mapendo Sheria yote hutimizwa.
11And this, knowing the time, that for us, the hour already [is] to be aroused out of sleep, for now nearer [is] our salvation than when we did believe;
11Zaidi ya hayo, ninyi mnajua tumo katika wakati gani: sasa ndio wakati wa kuamka usingizini; naam, wokovu wetu u karibu zaidi sasa kuliko wakati ule tulipoanza kuamini.
12the night did advance, and the day came nigh; let us lay aside, therefore, the works of the darkness, and let us put on the armour of the light;
12Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Basi, tutupilie mbali mambo yote ya giza, tukajitwalie silaha za mwanga.
13as in day-time, let us walk becomingly; not in revellings and drunkennesses, not in chamberings and lasciviousnesses, not in strife and emulation;
13Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mchana; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu.
14but put ye on the Lord Jesus Christ, and for the flesh take no forethought — for desires.
14Bwana Yesu Kristo awe vazi lenu; msishughulikie tena tamaa zenu za maumbile na kuziridhisha.