1وقال لتلاميذه لا يمكن الا ان تأتي العثرات. ولكن ويل للذي تأتي بواسطته.
1Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
2خير له لو طوق عنقه بحجر رحى وطرح في البحر من ان يعثر احد هؤلاء الصغار.
2Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.
3احترزوا لانفسكم. وان اخطأ اليك اخوك فوبخه. وان تاب فاغفر له.
3Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.
4وان اخطأ اليك سبع مرات في اليوم ورجع اليك سبع مرات في اليوم قائلا انا تائب فاغفر له.
4Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema Nimetubu, lazima umsamehe."
5فقال الرسل للرب زد ايماننا.
5Mitume wakamwambia Bwana, "Utuongezee imani."
6فقال الرب لو كان لكم ايمان مثل حبة خردل لكنتم تقولون لهذه الجميزة انقلعي وانغرسي في البحر فتطيعكم
6Naye Bwana akajibu, "Kama imani yenu ingekuwa ndogo hata kama chembe ndogo ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu: Ng'oka ukajipandikize baharini, nao ungewatii.
7ومن منكم له عبد يحرث او يرعى يقول له اذا دخل من الحقل تقدم سريعا واتكئ.
7"Tuseme mmoja wenu ana mtumishi ambaye analima shambani au anachunga kondoo. Je, anaporudi kutoka shambani, atamwambia: Haraka, njoo ule chakula?
8بل ألا يقول له اعدد ما اتعشى به وتمنطق واخدمني حتى آكل واشرب وبعد ذلك تأكل وتشرب انت.
8La! Atamwambia: Nitayarishie chakula, ujifunge tayari kunitumikia mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo nawe ule na unywe.
9فهل لذلك العبد فضل لانه فعل ما امر به لا اظن.
9Je utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?
10كذلك انتم ايضا متى فعلتم كل ما أمرتم به فقولوا اننا عبيد بطالون. لاننا انما عملنا ما كان يجب علينا
10Hali kadhalika na ninyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya."
11وفي ذهابه الى اورشليم اجتاز في وسط السامرة والجليل.
11Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia mipakani mwa Samaria na Galilaya.
12وفيما هو داخل الى قرية استقبله عشرة رجال برص فوقفوا من بعيد.
12Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.
13ورفعوا صوتا قائلين يا يسوع يا معلّم ارحمنا.
13Wakapaza sauti wakisema, "Yesu Mwalimu, tuonee huruma!"
14فنظر وقال لهم اذهبوا وأروا انفسكم للكهنة. وفيما هم منطلقون طهروا.
14Alipowaona akawaambia, "Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani." Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.
15فواحد منهم لما رأى انه شفي رجع يمجد الله بصوت عظيم.
15Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.
16وخرّ على وجهه عند رجليه شاكرا له. وكان سامريا.
16Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.
17فاجاب يسوع وقال أليس العشرة قد طهروا. فاين التسعة.
17Hapo Yesu akasema, "Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?
18ألم يوجد من يرجع ليعطي مجدا للّه غير هذا الغريب الجنس.
18Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?"
19ثم قال له قم وامض. ايمانك خلصك
19Halafu akamwambia huyo mtu, "Simama, uende zako; imani yako imekuponya."
20ولما سأله الفريسيون متى يأتي ملكوت الله اجابهم وقال لا يأتي ملكوت الله بمراقبة.
20Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, "Ufalme wa Mungu utakuja lini?" Naye akawajibu, "Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.
21ولا يقولون هوذا ههنا او هوذا هناك لان ها ملكوت الله داخلكم
21Wala hakuna atakayeweza kusema, Uko hapa, au Uko pale. Kwa kweli Ufalme wa Mungu uko kati yenu."
22وقال للتلاميذ ستأتي ايام فيها تشتهون ان تروا يوما واحدا من ايام ابن الانسان ولا ترون.
22Halafu akawaambia wanafunzi wake, "Siku zinakuja ambapo mtatamani kuona mojawapo ya siku za Mwana wa Mtu, lakini hamtaiona.
23ويقولون لكم هوذا ههنا او هوذا هناك. لا تذهبوا ولا تتبعوا.
23Na watu watawaambieni: Tazameni yuko hapa; ninyi msitoke wala msiwafuate.
24لانه كما ان البرق الذي يبرق من ناحية تحت السماء يضيء الى ناحية تحت السماء كذلك يكون ايضا ابن الانسان في يومه.
24Kwa maana kama vile umeme unavyotokea ghafla na kuangaza anga upande mmoja hadi mwingine, ndivyo Mwana wa Mtu atakavyokuwa siku yake.
25ولكن ينبغي اولا ان يتألم كثيرا ويرفض من هذا الجيل.
25Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.
26وكما كان في ايام نوح كذلك يكون ايضا في ايام ابن الانسان.
26Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.
27كانوا يأكلون ويشربون ويزوجون ويتزوجون الى اليوم الذي فيه دخل نوح الفلك وجاء الطوفان واهلك الجميع.
27Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.
28كذلك ايضا كما كان في ايام لوط كانوا يأكلون ويشربون ويشترون ويبيعون ويغرسون ويبنون.
28Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.
29ولكن اليوم الذي فيه خرج لوط من سدوم امطر نارا وكبريتا من السماء فاهلك الجميع.
29Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.
30هكذا يكون في اليوم الذي فيه يظهر ابن الانسان
30Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.
31في ذلك اليوم من كان على السطح وامتعته في البيت فلا ينزل ليأخذها. والذي في الحقل كذلك لا يرجع الى الوراء.
31"Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.
32اذكروا امرأة لوط.
32Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti.
33من طلب ان يخلّص نفسه يهلكها ومن اهلكها يحييها.
33Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.
34اقول لكم انه في تلك الليلة يكون اثنان على فراش واحد فيؤخذ الواحد ويترك الآخر.
34Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.
35تكون اثنتان تطحنان معا فتؤخذ الواحدة وتترك الاخرى.
35Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa."
36يكون اثنان في الحقل فيؤخذ الواحد ويترك الآخر.
36Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
37فاجابوا وقالوا له اين يا رب. فقال لهم حيث تكون الجثّة هناك تجتمع النسور
37Hapo wakamwuliza, "Ni wapi Bwana?" Naye akawaambia, "Ulipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia."