الكتاب المقدس (Van Dyke)

Swahili: New Testament

Mark

1

1بدء انجيل يسوع المسيح ابن الله
1Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2كما هو مكتوب في الانبياء. ها انا ارسل امام وجهك ملاكي الذي يهيّئ طريقك قدامك.
2Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3صوت صارخ في البرية اعدّوا طريق الرب اصنعوا سبله مستقيمة.
3Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake."
4كان يوحنا يعمد في البرية ويكرز بمعمودية التوبة لمغفرة الخطايا.
4Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5وخرج اليه جميع كورة اليهودية واهل اورشليم واعتمدوا جميعهم منه في نهر الاردن معترفين بخطاياهم.
5Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6وكان يوحنا يلبس وبر الابل ومنطقة من جلد على حقويه ويأكل جرادا وعسلا بريا.
6Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7وكان يكرز قائلا يأتي بعدي من هو اقوى مني الذي لست اهلا ان انحني واحل سيور حذائه.
7Naye alihubiri akisema, "Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8انا عمدتكم بالماء واما هو فسيعمدكم بالروح القدس
8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu."
9وفي تلك الايام جاء يسوع من ناصرة الجليل واعتمد من يوحنا في الاردن.
9Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10وللوقت وهو صاعد من الماء رأى السموات قد انشقت والروح مثل حمامة نازلا عليه.
10Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11وكان صوت من السموات. انت ابني الحبيب الذي به سررت
11Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
12وللوقت اخرجه الروح الى البرية.
12Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13وكان هناك في البرية اربعين يوما يجرب من الشيطان. وكان مع الوحوش. وصارت الملائكة تخدمه
13akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14وبعدما اسلم يوحنا جاء يسوع الى الجليل يكرز ببشارة ملكوت الله.
14Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15ويقول قد كمل الزمان واقترب ملكوت الله. فتوبوا وآمنوا بالانجيل
15"Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!"
16وفيما هو يمشي عند بحر الجليل ابصر سمعان واندراوس اخاه يلقيان شبكة في البحر. فانهما كانا صيادين.
16Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17فقال لهما يسوع هلم ورائي فاجعلكما تصيران صيادي الناس.
17Yesu akawaambia, "Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
18فللوقت تركا شباكهما وتبعاه.
18Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19ثم اجتاز من هناك قليلا فرأى يعقوب بن زبدي ويوحنا اخاه وهما في السفينة يصلحان الشباك.
19Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20فدعاهما للوقت. فتركا اباهما زبدي في السفينة مع الأجرى وذهبا وراءه
20Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21ثم دخلوا كفرناحوم وللوقت دخل المجمع في السبت وصار يعلم.
21Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22فبهتوا من تعليمه لانه كان يعلّمهم كمن له سلطان وليس كالكتبة.
22Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23وكان في مجمعهم رجل به روح نجس. فصرخ
23Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24قائلا آه ما لنا ولك يا يسوع الناصري. أتيت لتهلكنا. انا اعرفك من انت قدوس الله.
24akapaaza sauti, "Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!"
25فانتهره يسوع قائلا اخرس واخرج منه.
25Yesu akamkemea, "Nyamaza! Mtoke mtu huyu."
26فصرعه الروح النجس وصاح بصوت عظيم وخرج منه.
26Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27فتحيروا كلهم حتى سأل بعضهم بعضا قائلين ما هذا. ما هو هذا التعليم الجديد. لانه بسلطان يأمر حتى الارواح النجسة فتطيعه.
27Watu wote wakashangaa, wakaulizana, "Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!"
28فخرج خبره للوقت في كل الكورة المحيطة بالجليل
28Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29ولما خرجوا من المجمع جاءوا للوقت الى بيت سمعان واندراوس مع يعقوب ويوحنا.
29Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30وكانت حماة سمعان مضطجعة محمومة. فللوقت اخبروه عنها.
30Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31فتقدم واقامها ماسكا بيدها فتركتها الحمّى حالا وصارت تخدمهم.
31Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32ولما صار المساء اذ غربت الشمس قدموا اليه جميع السقماء والمجانين.
32Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33وكانت المدينة كلها مجتمعة على الباب.
33Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34فشفى كثيرين كانوا مرضى بامراض مختلفة واخرج شياطين كثيرة ولم يدع الشياطين يتكلمون لانهم عرفوه
34Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35وفي الصبح باكرا جدا قام وخرج ومضى الى موضع خلاء وكان يصلّي هناك.
35Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36فتبعه سمعان والذين معه.
36Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37ولما وجدوه قالوا له ان الجميع يطلبونك.
37Walipomwona wakamwambia, "Kila mtu anakutafuta."
38فقال لهم لنذهب الى القرى المجاورة لاكرز هناك ايضا لاني لهذا خرجت.
38Yesu akawaambia, "Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo."
39فكان يكرز في مجامعهم في كل الجليل ويخرج الشياطين
39Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40فأتى اليه ابرص يطلب اليه جاثيا وقائلا له ان اردت تقدر ان تطهرني.
40Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, "Ukitaka, waweza kunitakasa!"
41فتحنن يسوع ومد يده ولمسه وقال له اريد فاطهر.
41Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, "Nataka, takasika!"
42فللوقت وهو يتكلم ذهب عنه البرص وطهر.
42Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43فانتهره وارسله للوقت
43Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44وقال له انظر لا تقل لاحد شيئا بل اذهب أر نفسك للكاهن وقدّم عن تطهيرك ما أمر به موسى شهادة لهم.
44"Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
45واما هو فخرج وابتدأ ينادي كثيرا ويذيع الخبر حتى لم يعد يقدر ان يدخل مدينة ظاهرا بل كان خارجا في مواضع خالية وكانوا يأتون اليه من كل ناحية
45Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.