1ثم دخل ايضا الى المجمع. وكان هناك رجل يده يابسة.
1Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2فصاروا يراقبونه هل يشفيه في السبت. لكي يشتكوا عليه.
2Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3فقال للرجل الذي له اليد اليابسة قم في الوسط.
3Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, "Njoo hapa katikati."
4ثم قال لهم هل يحل في السبت فعل الخير او فعل الشر. تخليص نفس او قتل. فسكتوا.
4Kisha, akawauliza, "Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao hawakusema neno.
5فنظر حوله اليهم بغضب حزينا على غلاظة قلوبهم وقال للرجل مدّ يدك. فمدها فعادت يده صحيحة كالاخرى.
5Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, "Nyosha mkono wako!" Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6فخرج الفريسيون للوقت مع الهيرودسيين وتشاوروا عليه لكي يهلكوه
6Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7فانصرف يسوع مع تلاميذه الى البحر وتبعه جمع كثير من الجليل ومن اليهودية
7Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8ومن اورشليم ومن ادومية ومن عبر الاردن. والذين حول صور وصيدا جمع كثير اذ سمعوا كم صنع أتوا اليه.
8Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9فقال لتلاميذه ان تلازمه سفينة صغيرة لسبب الجمع كي لا يزحموه.
9Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10لانه كان قد شفى كثيرين حتى وقع عليه ليلمسه كل من فيه داء.
10Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11والارواح النجسة حينما نظرته خرّت له وصرخت قائلة انك انت ابن الله.
11Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, "Wewe ni Mwana wa Mungu!"
12واوصاهم كثيرا ان لا يظهروه
12Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13ثم صعد الى الجبل ودعا الذين ارادهم فذهبوا اليه.
13Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14واقام اثني عشر ليكونوا معه وليرسلهم ليكرزوا.
14naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15ويكون لهم سلطان على شفاء الامراض واخراج الشياطين.
15na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16وجعل لسمعان اسم بطرس.
16Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17ويعقوب بن زبدي ويوحنا اخا يعقوب وجعل لهما اسم بوانرجس اي ابني الرعد.
17Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake "wanangurumo"),
18واندراوس وفيلبس وبرثولماوس ومتى وتوما ويعقوب بن حلفى وتداوس وسمعان القانوي.
18Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19ويهوذا الاسخريوطي الذي اسلمه. ثم أتوا الى بيت.
19Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20فاجتمع ايضا جمع حتى لم يقدروا ولا على اكل خبز.
20Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21ولما سمع اقرباؤه خرجوا ليمسكوه لانهم قالوا انه مختل.
21Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22واما الكتبة الذين نزلوا من اورشليم فقالوا ان معه بعلزبول. وانه برئيس الشياطين يخرج الشياطين.
22Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, "Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo."
23فدعاهم وقال لهم بامثال كيف يقدر شيطان ان يخرج شيطانا.
23Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, "Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24وان انقسمت مملكة على ذاتها لا تقدر تلك المملكة ان تثبت.
24Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25وان انقسم بيت على ذاته لا يقدر ذلك البيت ان يثبت.
25Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26وان قام الشيطان على ذاته وانقسم لا يقدر ان يثبت بل يكون له انقضاء.
26Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27لا يستطيع احد ان يدخل بيت قوي وينهب امتعته ان لم يربط القوي اولا وحينئذ ينهب بيته.
27"Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28الحق اقول لكم ان جميع الخطايا تغفر لبني البشر والتجاديف التي يجدفونها.
28"Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29ولكن من جدّف على الروح القدس فليس له مغفرة الى الابد بل هو مستوجب دينونة ابدية.
29lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele."
30لانهم قالوا ان معه روحا نجسا
30(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, "Ana pepo mchafu.")
31فجاءت حينئذ اخوته وامه ووقفوا خارجا وارسلوا اليه يدعونه.
31Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32وكان الجمع جالسا حوله فقالوا له هوذا امك واخوتك خارجا يطلبونك.
32Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona."
33فاجابهم قائلا من امي واخوتي.
33Yesu akawaambia, "Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?"
34ثم نظر حوله الى الجالسين وقال ها امي واخوتي.
34Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, "Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35لان من يصنع مشيئة الله هو اخي واختي وامي
35Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu."