الكتاب المقدس (Van Dyke)

Swahili: New Testament

Matthew

24

1ثم خرج يسوع ومضى من الهيكل . ‎ فتقدم تلاميذه لكي يروه ابنية الهيكل.
1Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
2فقال لهم يسوع أما تنظرون جميع هذه. الحق اقول لكم انه لا يترك ههنا حجر على حجر لا ينقض
2Yesu akawaambia, "Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
3وفيما هو جالس على جبل الزيتون تقدم اليه التلاميذ على انفراد قائلين قل لنا متى يكون هذا وما هي علامة مجيئك وانقضاء الدهر.
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?"
4فاجاب يسوع وقال لهم انظروا لا يضلكم احد.
4Yesu akawajibu, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5فان كثيرين سيأتون باسمي قائلين انا هو المسيح ويضلون كثيرين.
5Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
6وسوف تسمعون بحروب واخبار حروب. انظروا لا ترتاعوا. لانه لا بد ان تكون هذه كلها. ولكن ليس المنتهى بعد.
6Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7لانه تقوم امة على امة ومملكة على مملكة وتكون مجاعات واوبئة وزلازل في اماكن.
7Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
8ولكن هذه كلها مبتدأ الاوجاع.
8Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9حينئذ يسلمونكم الى ضيق ويقتلونكم وتكونون مبغضين من جميع الامم لاجل اسمي.
9"Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
10وحينئذ يعثر كثيرون ويسلمون بعضهم بعضا ويبغضون بعضهم بعضا.
10Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
11ويقوم انبياء كذبة كثيرون ويضلون كثيرين.
11Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
12ولكثرة الاثم تبرد محبة الكثيرين.
12Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
13ولكن الذي يصبر الى المنتهى فهذا يخلص.
13Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.
14ويكرز ببشارة الملكوت هذه في كل المسكونة شهادة لجميع الامم. ثم يأتي المنتهى
14Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
15فمتى نظرتم رجسة الخراب التي قال عنها دانيال النبي قائمة في المكان المقدس. ليفهم القارئ.
15"Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
16فحينئذ ليهرب الذين في اليهودية الى الجبال.
16hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.
17والذي على السطح فلا ينزل لياخذ من بيته شيئا.
17Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
18والذي في الحقل فلا يرجع الى ورائه لياخذ ثيابه.
18Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
19وويل للحبالى والمرضعات في تلك الايام.
19Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
20وصلّوا لكي لا يكون هربكم في شتاء ولا في سبت.
20Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
21لانه يكون حينئذ ضيق عظيم لم يكن مثله منذ ابتداء العالم الى الآن ولن يكون.
21Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
22ولو لم تقصّر تلك الايام لم يخلص جسد. ولكن لاجل المختارين تقصّر تلك الايام.
22Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23حينئذ ان قال لكم احد هوذا المسيح هنا او هناك فلا تصدقوا.
23"Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
24لانه سيقوم مسحاء كذبة وانبياء كذبة ويعطون آيات عظيمة وعجائب حتى يضلوا لو امكن المختارين ايضا.
24Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
25ها انا قد سبقت واخبرتكم.
25Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.
26فان قالوا لكم ها هو في البرية فلا تخرجوا. ها هو في المخادع فلا تصدقوا.
26Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
27لانه كما ان البرق يخرج من المشارق ويظهر الى المغارب هكذا يكون ايضا مجيء ابن الانسان.
27maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
28لانه حيثما تكن الجثّة فهناك تجتمع النسور
28Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29وللوقت بعد ضيق تلك الايام تظلم الشمس والقمر لا يعطي ضؤه والنجوم تسقط من السماء وقوات السموات تتزعزع.
29"Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
30وحينئذ تظهر علامة ابن الانسان في السماء. وحينئذ تنوح جميع قبائل الارض ويبصرون ابن الانسان آتيا على سحاب السماء بقوة ومجد كثير.
30Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
31فيرسل ملائكته ببوق عظيم الصوت فيجمعون مختاريه من الاربع الرياح من اقصاء السموات الى اقصائها.
31Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
32فمن شجرة التين تعلّموا المثل متى صار غصنها رخصا واخرجت اوراقها تعلمون ان الصيف قريب.
32"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33هكذا انتم ايضا متى رأيتم هذا كله فاعلموا انه قريب على الابواب.
33Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
34الحق اقول لكم لا يمضي هذا الجيل حتى يكون هذا كله.
34Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
35السماء والارض تزولان ولكن كلامي لا يزول.
35Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36واما ذلك اليوم وتلك الساعة فلا يعلم بهما احد ولا ملائكة السموات الا ابي وحده.
36"Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
37وكما كانت ايام نوح كذلك يكون ايضا مجيء ابن الانسان.
37Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
38لانه كما كانوا في الايام التي قبل الطوفان ياكلون ويشربون ويتزوجون ويزوّجون الى اليوم الذي دخل فيه نوح الفلك
38Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
39ولم يعلموا حتى جاء الطوفان واخذ الجميع. كذلك يكون ايضا مجيء ابن الانسان.
39Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
40حينئذ يكون اثنان في الحقل. يؤخذ الواحد ويترك الآخر.
40Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
41اثنتان تطحنان على الرحى. تؤخذ الواحدة وتترك الآخرى
41Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
42اسهروا اذا لانكم لا تعلمون في اية ساعة يأتي ربكم.
42Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
43واعلموا هذا انه لو عرف رب البيت في اية هزيع يأتي السارق لسهر ولم يدع بيته ينقب.
43Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
44لذلك كونوا انتم ايضا مستعدين لانه في ساعة لا تظنون يأتي ابن الانسان.
44Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
45فمن هو العبد الامين الحكيم الذي اقامه سيده على خدمه ليعطيهم الطعام في حينه.
45Yesu akaendelea kusema, "Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
46طوبى لذلك العبد الذي اذا جاء سيده يجده يفعل هكذا.
46Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47الحق اقول لكم انه يقيمه على جميع امواله.
47Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48ولكن ان قال ذلك العبد الردي في قلبه سيدي يبطئ قدومه.
48Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
49فيبتدئ يضرب العبيد رفقاءه ويأكل ويشرب مع السكارى.
49kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50يأتي سيد ذلك العبد في يوم لا ينتظره وفي ساعة لا يعرفها.
50bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51فيقطّعه ويجعل نصيبه مع المرائين. هناك يكون البكاء وصرير الاسنان
51Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.