American Standard Version

Swahili: New Testament

1 Timothy

2

1I exhort therefore, first of all, that supplications, prayers, intercessions, thanksgivings, be made for all men;
1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2for kings and all that are in high place; that we may lead a tranquil and quiet life in all godliness and gravity.
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3This is good and acceptable in the sight of God our Saviour;
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4who would have all men to be saved, and come to the knowledge of the truth.
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5For there is one God, one mediator also between God and men, [himself] man, Christ Jesus,
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6who gave himself a ransom for all; the testimony [to be borne] in its own times;
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7whereunto I was appointed a preacher and an apostle (I speak the truth, I lie not), a teacher of the Gentiles in faith and truth.
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8I desire therefore that the men pray in every place, lifting up holy hands, without wrath and disputing.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9In like manner, that women adorn themselves in modest apparel, with shamefastness and sobriety; not with braided hair, and gold or pearls or costly raiment;
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10but (which becometh women professing godliness) through good works.
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11Let a woman learn in quietness with all subjection.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12But I permit not a woman to teach, nor to have dominion over a man, but to be in quietness.
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13For Adam was first formed, then Eve;
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14and Adam was not beguiled, but the woman being beguiled hath fallen into transgression:
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15but she shall be saved through her child-bearing, if they continue in faith and love and sanctification with sobriety.
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.