American Standard Version

Swahili: New Testament

Colossians

3

1If then ye were raised together with Christ, seek the things that are above, where Christ is, seated on the right hand of God.
1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
2Set your mind on the things that are above, not on the things that are upon the earth.
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
3For ye died, and your life is hid with Christ in God.
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4When Christ, [who is] our life, shall be manifested, then shall ye also with him be manifested in glory.
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5Put to death therefore your members which are upon the earth: fornication, uncleanness, passion, evil desire, and covetousness, which is idolatry;
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
6for which things' sake cometh the wrath of God upon the sons of disobedience:
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
7wherein ye also once walked, when ye lived in these things;
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
8but now do ye also put them all away: anger, wrath, malice, railing, shameful speaking out of your mouth:
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
9lie not one to another; seeing that ye have put off the old man with his doings,
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
10and have put on the new man, that is being renewed unto knowledge after the image of him that created him:
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
11where there cannot be Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, bondman, freeman; but Christ is all, and in all.
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12Put on therefore, as God's elect, holy and beloved, a heart of compassion, kindness, lowliness, meekness, longsuffering;
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13forbearing one another, and forgiving each other, if any man have a complaint against any; even as the Lord forgave you, so also do ye:
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
14and above all these things [put on] love, which is the bond of perfectness.
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
15And let the peace of Christ rule in your hearts, to the which also ye were called in one body; and be ye thankful.
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
16Let the word of Christ dwell in you richly; in all wisdom teaching and admonishing one another with psalms [and] hymns [and] spiritual songs, singing with grace in your hearts unto God.
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
17And whatsoever ye do, in word or in deed, [do] all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father through him.
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
18Wives, be in subjection to your husbands, as is fitting in the Lord.
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
19Husbands, love your wives, and be not bitter against them.
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
20Children, obey your parents in all things, for this is well-pleasing in the Lord.
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
21Fathers, provoke not your children, that they be not discouraged.
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
22Servants, obey in all things them that are your masters according to the flesh; not with eye-service, as men-pleasers, but in singleness of heart, fearing the Lord:
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
23whatsoever ye do, work heartily, as unto the Lord, and not unto men;
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
24knowing that from the Lord ye shall receive the recompense of the inheritance: ye serve the Lord Christ.
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
25For he that doeth wrong shall receive again for the wrong that he hath done: and there is no respect of persons.
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.