American Standard Version

Swahili: New Testament

Hebrews

3

1Wherefore, holy brethren, partakers of a heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession, [even] Jesus;
1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2who was faithful to him that appointed him, as also was Moses in all his house.
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3For he hath been counted worthy of more glory than Moses, by so much as he that built the house hath more honor than the house.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4For every house is builded by some one; but he that built all things is God.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were afterward to be spoken;
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6but Christ as a son, over his house; whose house are we, if we hold fast our boldness and the glorying of our hope firm unto the end.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7Wherefore, even as the Holy Spirit saith, To-day if ye shall hear his voice,
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8Harden not your hearts, as in the provocation, Like as in the day of the trial in the wilderness,
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9Where your fathers tried [me] by proving [me,] And saw my works forty years.
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10Wherefore I was displeased with this generation, And said, They do always err in their heart: But they did not know my ways;
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11As I sware in my wrath, They shall not enter into my rest.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
12Take heed, brethren, lest haply there shall be in any one of you an evil heart of unbelief, in falling away from the living God:
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13but exhort one another day by day, so long as it is called To-day; lest any one of you be hardened by the deceitfulness of sin:
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14for we are become partakers of Christ, if we hold fast the beginning of our confidence firm unto the end:
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15while it is said, To-day if ye shall hear his voice, Harden not your hearts, as in the provocation.
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
16For who, when they heard, did provoke? nay, did not all they that came out of Egypt by Moses?
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17And with whom was he displeased forty years? was it not with them that sinned, whose bodies fell in the wilderness?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18And to whom sware he that they should not enter into his rest, but to them that were disobedient?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19And we see that they were not able to enter in because of unbelief.
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.