1Now when morning was come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus to put him to death:
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2and they bound him, and led him away, and delivered him up to Pilate the governor.
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3Then Judas, who betrayed him, when he saw that he was condemned, repented himself, and brought back the thirty pieces of silver to the chief priests and elders,
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4saying, I have sinned in that I betrayed innocent blood. But they said, What is that to us? see thou [to it].
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
5And he cast down the pieces of silver into the sanctuary, and departed; and he went away and hanged himself.
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6And the chief priests took the pieces of silver, and said, It is not lawful to put them into the treasury, since it is the price of blood.
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
7And they took counsel, and bought with them the potter's field, to bury strangers in.
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8Wherefore that field was called, the field of blood, unto this day.
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9Then was fulfilled that which was spoken through Jeremiah the prophet, saying, And they took the thirty pieces of silver, the price of him that was priced, whom [certain] of the children of Israel did price;
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10and they gave them for the potter's field, as the Lord appointed me.
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
11Now Jesus stood before the governor: and the governor asked him, saying, Art thou the King of the Jews? And Jesus said unto him, Thou sayest.
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
12And when he was accused by the chief priests and elders, he answered nothing.
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13Then saith Pilate unto him, Hearest thou not how many things they witness against thee?
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
14And he gave him no answer, not even to one word: insomuch that the governor marvelled greatly.
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15Now at the feast the governor was wont to release unto the multitude one prisoner, whom they would.
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16And they had then a notable prisoner, called Barabbas.
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17When therefore they were gathered together, Pilate said unto them, Whom will ye that I release unto you? Barabbas, or Jesus who is called Christ?
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
18For he knew that for envy they had delivered him up.
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19And while he was sitting on the judgment-seat, his wife sent unto him, saying, Have thou nothing to do with that righteous man; for I have suffered many things this day in a dream because of him.
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
20Now the chief priests and the elders persuaded the multitudes that they should ask for Barabbas, and destroy Jesus.
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21But the governor answered and said unto them, Which of the two will ye that I release unto you? And they said, Barabbas.
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
22Pilate saith unto them, What then shall I do unto Jesus who is called Christ? They all say, Let him be crucified.
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
23And he said, Why, what evil hath he done? But they cried out exceedingly, saying, Let him be crucified.
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
24So when Pilate saw that he prevailed nothing, but rather that a tumult was arising, he took water, and washed his hands before the multitude, saying, I am innocent of the blood of this righteous man; see ye [to it].
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
25And all the people answered and said, His blood [be] on us, and on our children.
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
26Then released he unto them Barabbas; but Jesus he scourged and delivered to be crucified.
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27Then the soldiers of the governor took Jesus into the Praetorium, and gathered unto him the whole band.
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28And they stripped him, and put on him a scarlet robe.
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29And they platted a crown of thorns and put it upon his head, and a reed in his right hand; and they kneeled down before him, and mocked him, saying, Hail, King of the Jews!
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
30And they spat upon him, and took the reed and smote him on the head.
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31And when they had mocked him, they took off from him the robe, and put on him his garments, and led him away to crucify him.
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32And as they came out, they found a man of Cyrene, Simon by name: him they compelled to go [with them], that he might bear his cross.
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33And they were come unto a place called Golgotha, that is to say, The place of a skull,
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
34they gave him wine to drink mingled with gall: and when he had tasted it, he would not drink.
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35And when they had crucified him, they parted his garments among them, casting lots;
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36and they sat and watched him there.
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37And they set up over his head his accusation written, THIS IS JESUS THE KING OF THE JEWS.
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
38Then are there crucified with him two robbers, one on the right hand and one on the left.
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39And they that passed by railed on him, wagging their heads,
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40and saying, Thou that destroyest the temple, and buildest it in three days, save thyself: if thou art the Son of God, come down from the cross.
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
41In like manner also the chief priests mocking [him], with the scribes and elders, said,
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42He saved others; himself he cannot save. He is the King of Israel; let him now come down from the cross, and we will believe on him.
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43He trusteth on God; let him deliver him now, if he desireth him: for he said, I am the Son of God.
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
44And the robbers also that were crucified with him cast upon him the same reproach.
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45Now from the sixth hour there was darkness over all the land until the ninth hour.
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46And about the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, Eli, Eli, lama sabachthani? that is, My God, my God, why hast thou forsaken me?
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
47And some of them stood there, when they heard it, said, This man calleth Elijah.
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
48And straightway one of them ran, and took a sponge, and filled it with vinegar, and put it on a reed, and gave him to drink.
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49And the rest said, Let be; let us see whether Elijah cometh to save him.
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
50And Jesus cried again with a loud voice, and yielded up his spirit.
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51And behold, the veil of the temple was rent in two from the top to the bottom; and the earth did quake; and the rocks were rent;
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52and the tombs were opened; and many bodies of the saints that had fallen asleep were raised;
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53and coming forth out of the tombs after his resurrection they entered into the holy city and appeared unto many.
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54Now the centurion, and they that were with him watching Jesus, when they saw the earthquake, and the things that were done, feared exceedingly, saying, Truly this was the Son of God.
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
55And many women were there beholding from afar, who had followed Jesus from Galilee, ministering unto him:
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James and Joses, and the mother of the sons of Zebedee.
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57And when even was come, there came a rich man from Arimathaea, named Joseph, who also himself was Jesus' disciple:
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58this man went to Pilate, and asked for the body of Jesus. Then Pilate commanded it to be given up.
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59And Joseph took the body, and wrapped it in a clean linen cloth,
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60and laid it in his own new tomb, which he had hewn out in the rock: and he rolled a great stone to the door of the tomb, and departed.
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61And Mary Magdalene was there, and the other Mary, sitting over against the sepulchre.
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62Now on the morrow, which is [the day] after the Preparation, the chief priests and the Pharisees were gathered together unto Pilate,
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63saying, Sir, we remember that that deceiver said while he was yet alive, After three days I rise again.
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64Command therefore that the sepulchre be made sure until the third day, lest haply his disciples come and steal him away, and say unto the people, He is risen from the dead: and the last error will be worse than the first.
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
65Pilate said unto them, Ye have a guard: go, make it [as] sure as ye can.
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
66So they went, and made the sepulchre sure, sealing the stone, the guard being with them.
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.