Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Matthew

23

1AYO nae si Jesus, jacuentuse y linajyan taotao, yan y disipuluña sija,
1Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2Ylegña: Y escriba yan y Fariseo sija manmatatachong gui tachong Moises;
2"Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
3Todo y mansinangane jamyo na inadaje, fatinas yan adaje; lao chamiyo fumatitinas taegüije y finatinasñiñija, sa sija jasasangan, lao ti jafatitinas.
3Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4Sa manmangogode catga sija na manmacat ya mapot machule, ya japolo gui jilo y apagan y taotao sija; lao sija ni y calalotñija ti manmalago janacalamten.
4Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5Lao todo y chechoñija, jafatinas para umalie ni y taotao sija sa janaancho y filacteriañija, ya jajujuto y madoblan y magagonñija.
5Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
6Ya yañija y finenana na saga gui guipot, yan y finenana na tachong gui sinagoga;
6Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
7Yan y manmasaluda gui plasa, yan ufanmafanaan ni y taotao sija, Rabi.
7Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
8Lao jamyo chamiyo fanmalalago manmafanaan. Rabi; sa unoja Maestronmiyo, ya todo jamyo mañelo.
8Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
9Chamiyo fanmamananaan ni uno tatanmiyo gui tano; sa unoja Tatanmiyo, na gaegue gui langet.
9Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
10Ni infanmamanaan uno amunmiyo; sa unoja amunmiyo, si Cristo.
10Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
11Lao y mas dangculo guiya jamyo, güiya utentagonmiyo.
11Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12Sa jayeja y munadangculon namae sagüe, umumitde; ya jayeja y munaumitden namaesagüe, güiya udangculo.
12Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
13¶ Lao ay ay para jamyo escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa injichom y raenon langet gui menan y taotao sija; ya ni jamyo ti manjalom, ni y para ufanjalom ti inpelo na ufanjalom.
13"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
14(Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa inticho y guima y biuda sija yan inagó y tinaetae; pot este inresibe dangculo na sentensia.)
14Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa inlilicue y tase yan y tano para infatinas un prosélito, ya anae esta infatinas, infatitinas güe lalajin sasalaguan dosbiaje mas qui jamyo.
15"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe.
16¶ Ay ay para jamyo, bachet na guia sija ni y ilegmiyo: Jayeja y manjula pot templo, taya este; lao jayeja y manjula pot y oron y templo, gaeisao güe.
16"Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
17Manbababa yan manbachet! Jafa mas dangculo, y oro pat y templo, ni y munasantos y oro?
17Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18Ya jayeja y manjula pot y attat, taya este; lao jayeja y manjula pot y ninae ni gaegue gui jiloña, gaeisao güe.
18Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19Manbachet jamyo! Jafa mas dangculo, y ninae pat y attat ni munasantos y ninae?
19Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20Enao mina y manjula pot y attat, manjula pot ayo yan todo y guaja gui jiloña.
20Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
21Ya y manjula pot y templo, manjula pot ayo yan pot güiya y sumaga gui jinalomña.
21Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
22Ya y manjula pot y langet, manjula pot y trono Yuus, yan pot güiya ni gaegue na matatachong gui jiloña.
22Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
23¶ Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa manmanapase jamyo diesmo y yetba buena, yan anis yan comino, ya inpelo y mas dangculo gui lay; y juisio, y minaase, yan y jinenggue. Este nesesita umafatinas, ya munga mapolo na ti infatinas y otro sija.
23Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24Bachet jamyo na guia sija! sa inguicula y ñamo, ya inpapañot y cameyo.
24Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
25¶ Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa infagagase y sumanjiyeng y posuelo yan y plato; lao y sumanjalom bula inamot yan minampos.
25"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
26Fariseo bachet jao! fagase finena y sumanjalom gui posuelo yan y plato, ya despues y sumanjiyong ugasgas locue.
26Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
27¶ Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa manparejo jamyo yan y manmablanquea na naftan na y sanjiyongña magajet na mauleg malie: lao y sumanjalomña bula tolang manmatae, yan todo y ináplacha.
27"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28Taegüenao locue jamyo y sumanjiyong magajet na manunas malie jamyo ni taotao sija; lao y sumanjalom bula hipocresia yan inechong.
28Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29¶ Ay ay para jamyo escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa infatinas naftan y profeta sija, ya inadotna y naftan y manunas,
29"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30Ya ilegmiyo: Yaguin mangaeguejam gui jaanin y tatanmame sija, ti infangachong yan sija gui jâgâ y profeta sija.
30Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
31Ayo mina jamyo mismo innae testimonio contra jamyo, na jamyo famaguon ayo sija y pumuno y profeta sija.
31Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
32Jamyo locue innabula y medidan y tatanmiyo.
32Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33Colebla sija, rasan colebla sija! Jaf taemano jamyo insujaye gui sentensian sasalaguan?
33Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu?
34¶ Enaomina estagüeyo na junae jamyo profeta sija, yan manmalate yan escribasija; ya palo guiya sija inpino ya inatane gui quiluus; ya y palo guiya sija, inpanag gui sinagoganmiyo, ya inpetsigue sija guinin siuda asta siuda;
34Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35Para ufato gui jilomiyo todo y tunas na jâgâ ni y machuda gui jilo y tano, desde y jâgân Abel y tinas, asta y jâgâ Sacharias, lajin Barachias, ni inpino gui entalo templo yan y attat.
35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36Magajet jusagane jamyo, na todo estesija ufanmato gui jilo este na generasion.
36Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
37¶ Jerusalem! Jerusalem! ni y pumuno y profeta sija, ni infagas ni acho todo y manmatago para jago, cuanto biaje malagoyo na jurecoje y famaguonmo, calang y ponedera yan jarecoje y poyitasña sija gui papa papaña, lao ti manmalago jamyo!
37"Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
38Estagüe na madingo guiya jamyo y guimanmiyo na ti mataotagüe.
38Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39Sa guajo jamyo sumangane, na desde pago, ti inliiyo, asta qui ilegmiyo: Dichoso güe y mato. pot y naan y Señot.
39Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."