1AYO nae y raenon langet parejo yan dies na bitgen, ni jachule y lamparañija ya manmapos para ujatagam y nobio.
1"Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2Ya y sinco guiya sija manmejnalom, ya y sinco manaetiningo.
2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3Y manaetiningo, jachule y lamparañija, ya ti manmañule laña.
3Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4Lao y manmejnalom manmañule laña gui baso, yan y lamparañija.
4Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5Ya anae atrasasao y nobio, manmatujog todo sija, ya manmaego.
5Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6Ya y tatalopuenge majungog un inagang, na ilegña: Estagüe y nobio na mamamaela! fanjuyong ya inresibe!
6Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7Ayo nae todo y bitgen sija mangajulo ya jafamauleg y lamparañija.
7Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8Ya y manaetiningo ilegñija ni manmejnalom: Naejam gui lañanmiyo sa y lamparanmame manmatae.
8Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9Ya y manmejnalom manmanope ilegñija: Munga sa ti mannajongjit; lao janao fanmalag y manmanbebende ya infanmamajan para jamyo namaesa.
9Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10Ya anae manmapos sija para ufanmamajan, mato y nobio; ya y estaba manlisto manjalom yan güiya gui guipot umasagua; ya majuchom y petta.
10Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11Despues manmato y palo na bitgen ya ilegñija: Señot, Señot, babayejam.
11Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12Lao güiya manope, ilegna; Magajet jusangane jamyo na ti jutungo jamyo.
12Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."
13Fanmagmata sa ti intingo y jaane ni y ora.
13Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14¶ Sa uguaja parejo yan un taotao ni jumanao chago na tano, ya jaagang antes y tentagoña sija, ya jaentrega sija ni güinajaña.
14"Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15Ya y uno janae sinco talento, ya y otro dos, ya y otro uno; ya cada uno taemano y guinefuloña; ya enseguidas mapos.
15Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16Ya y rumesibe y sinco na talento, janacometsio, ya jagana talo sinco na talento.
16Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17Parejo locue yan y rumesibe dos, mangana talo dos.
17Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18Lao y rumesibe y uno, jumuyong ya jaguadog y eda, ya janaatog y salape y senotña.
18Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19Despues di apmam na tiempo, mato y señot ayo sija na tentago, ya manacuentas yan sija.
19"Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20Ya mato ayo y rumesibe sinco na talento, yan mañuñule talo sinco talento, ya ilegña: Señot, sinco na talento unnaeyo; estagüe talo sinco na junafangana.
20Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21Y senotña ilegña nu güiya: Mauleg chechomo, jago mauleg na tentago yan guesmanosguejao: guine unfatinas mauleg gui didide, bae jupoluyejao megae: jalom gui minagof y señotmo.
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22Mato locue ayo y rumesibe dos na talento, ya ilegña: Señot, dos na talento unnaeyo; estagüe talo dos talento na junafangana.
22"Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23Y señotña ilegña nu güiya: Mauleg chechomo, jago mauleg na tentago yan guesmanosguejao: guine unfatinas mauleg gui didide, bae jupoluyejao megae; jalom gui minagof y señotmo.
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24Mato locue ayo y rumesibe un talento, ya ilegña: Señot, guajo jutungo na jago majetogjao na taotao; sa mangongoco jao gui anae ti mananom jao, ya manrecocoje jao gui anae ti mañalapon jao;
24"Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25Ya maañaoyo, ya maposyo ya junaatog y talentomo gui jalom y tano: estagüe ni iyomo.
25Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26Lao y señotña inepe güe ilegña: Taelayejao na tentago yan gago. Untungoja na mangongoco yo gui anae ti mananom yo, ya manrecocoje yo gui anae ti mañalapon yo;
26"Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27Enao mina jago nesesita unnae y banquero sija ni salapejo, ya yaguin matoyo, juresibe y iyoco yan ganansia.
27Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28Enao mina umanajanao ayo na talento guiya güiya, ya umannae ayo y guaja dies na talento.
28Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29Sa jayeja y guaja, umannae güe, ya uguaja megae; lao y taya iyoña, achogja guaja güinajaña umanajanao.
29Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30Ya y taebalenña na tentago, yute juyong gui jalom jomjom, ayo nae uguaja tumanges yan chegcheg nifen.
30Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31¶ Yaguin y Lajin taotao mato gui minalagña, yan todo y angjetña sija, ayo nae ufatachong gui jilo y tachong y minalagña;
31"Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32Ya umanafandaña gui menaña todo y nasion sija; ya umanafañajnge y uno gui otro, calang y pastot yan janasajnge y quinilo sija gui chiba;
32na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33Ya japolo y quinilo sija gui agapaña, ya y chiba gui acagüeña.
33Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34Ayo nae y ray ualog ni mangaegue gui agapaña: Maela jamyo mandichoso gui Tatajo, ya inereda y raeno ni esta listo para jamyo desde y mafatinas y tano;
34"Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35Sa anae ñalangyo, innachocho yo; anae majoyo, innaguimen yo; anae taotaojuyong yo, innajalom yo;
35Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36Anae taya magagojo, innaminagago yo. Anae malangoyo, inbesita yo; anae gaegue yo gui calaboso, manmato jamyo guiya guajo.
36nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37Ayo nae y manunas manmanope güe ilegñija: Señot, ngaean nae inliijao ñalang, ya innachocho jao? pat majo, ya innaguimen jao?
37Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38Ngaean nae inliijao taotaojuyong, ya innajalom jao? pat anae taya magagomo, ya innaminagago jao?
38Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39Pat ñgaean nae inliijao malango, pat y calaboso, ya manmatojam guiya jago?
39Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40Y ray ujaope ilegña nu sija: Magajet jusangane jamyo, taemanoja na y infatinas ni uno güine gui mandiquique na mañelujo, infatinasja locue nu guajo.
40Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41Ayo nae ilegña locue ni y mangaegue gui acagüeña: Fanjanao guiya guajo, jamyo matdito, fanmalag y taejinecog na guafe, ni esta manalisto ni anite yan y anjetña sija;
41"Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.
42Sa anae ñalangyo, ti innachocho yo; anae majoyo, ti innaguimen yo;
42Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43Anae taotaojuyong yo, ti innajalom yo; anae taya magagojo, ti innaminagago yo; malangoyo, yan gaegue yo gui calaboso, lao ti inbesita yo.
43Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44Ayo nae ufanmanope locue sija, ilegñija: Señot, ngaean nae inliijao ñalang, pat majo, pat taotaojuyong, pat taya magagomo, pat malango, pat gui calaboso, ya ti insetbejao?
44"Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45Ayo nae ujaope sija, ilegña: Magajet jusangane jamyo, na taemanoja ti infatinas nu uno güine gui mas mandiquique, ti infatinas nu guajo.
45Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46Ya esta sija manmapos para y taejinecog na minasapet; lao y manunas para y taejinecog na linala.
46Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."